Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Polisi waua jambazi Mwanza
Habari Mchanganyiko

Polisi waua jambazi Mwanza

Spread the love

MTU mmoja aliyefahamika kwa jina la Seleman Israel ‘Akayesu’ (54) anayetuhumiwa kuwa jambazi amefariki dunia kwa kupigwa risasi wakati akijaribu kuwatoroka askari polisi wilaya ya Nyamagana Mkoani Mwanza. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mwanza … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Julai 24, 2018 kwa vyombo na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, DCP Ahmed Msangi .

Akielezea tukio hilo, DCP Msangi amesema lilitokea alfajiri ya leo kwenye maeneo ya Luchelele wilayani Nyamagana, ambapo marehemu Akayesu pamoja na mwenzake anayefahamika kwa jina la Salivatory Emmanuel ‘Katiyari’ walikamatwa na polisi kwa tuhuma za kujihusisha na ujambazi wa kutumia silaha.

DCP Msangi amesema majambazi hao baada ya kufanyiwa mahojiano walikiri kuhusika katika matukio mbalimbali ikiwemo tukio la mauaji ya mlinzi aliyekuwa lindoni maeneo ya Igombe mkoani humo.

“Baada ya majambazi hao kukamatwa walifanyiwa mahojiano na polisi na kukiri kuwa na silaha wanayotumia katika uhalifu na wameificha maeneo ya Luchelele, askari waliongozana na whaalifu hao hadi eneo hilo na baada ya kuitoa walikurupuka na kuanza kukimbia,” amesema.

Kamanda Msangi ametoa onyo kwa wakazi wa mkoa wa Mwanza hasa vijana kuacha tabia ya kujihusisha na uhalifu na kuwaomba raia wema kuendelea kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi ililiweze kudhibiti uhalifu mkoani humo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!