Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Polisi waua jambazi Mwanza
Habari Mchanganyiko

Polisi waua jambazi Mwanza

Spread the love

MTU mmoja aliyefahamika kwa jina la Seleman Israel ‘Akayesu’ (54) anayetuhumiwa kuwa jambazi amefariki dunia kwa kupigwa risasi wakati akijaribu kuwatoroka askari polisi wilaya ya Nyamagana Mkoani Mwanza. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mwanza … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Julai 24, 2018 kwa vyombo na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, DCP Ahmed Msangi .

Akielezea tukio hilo, DCP Msangi amesema lilitokea alfajiri ya leo kwenye maeneo ya Luchelele wilayani Nyamagana, ambapo marehemu Akayesu pamoja na mwenzake anayefahamika kwa jina la Salivatory Emmanuel ‘Katiyari’ walikamatwa na polisi kwa tuhuma za kujihusisha na ujambazi wa kutumia silaha.

DCP Msangi amesema majambazi hao baada ya kufanyiwa mahojiano walikiri kuhusika katika matukio mbalimbali ikiwemo tukio la mauaji ya mlinzi aliyekuwa lindoni maeneo ya Igombe mkoani humo.

“Baada ya majambazi hao kukamatwa walifanyiwa mahojiano na polisi na kukiri kuwa na silaha wanayotumia katika uhalifu na wameificha maeneo ya Luchelele, askari waliongozana na whaalifu hao hadi eneo hilo na baada ya kuitoa walikurupuka na kuanza kukimbia,” amesema.

Kamanda Msangi ametoa onyo kwa wakazi wa mkoa wa Mwanza hasa vijana kuacha tabia ya kujihusisha na uhalifu na kuwaomba raia wema kuendelea kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi ililiweze kudhibiti uhalifu mkoani humo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!