Wednesday , 1 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali inawasurubu askari Magereza
Habari za SiasaTangulizi

Serikali inawasurubu askari Magereza

Askari Magereza wakiwa katika maonesho jinsi wanavyomdhibiti mfungwa mkorofi
Spread the love

JOSEPH Mbilinyi ‘Sugu’ Mbunge wa jimbo la Mbeya Mjini (Chadema) ameing’ang’ania serikali kwenye suala la mustakabali wa mafao ya askari Magereza. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Sugu akiuliza swali la nyongeza kwa Naibu Waziri wa Fedha Dk. Ashatu Kijaji amesema kuwa askari magereza wanafanya kazi ngumu ya kulinda wahalifu lakini wanapostaafu serikali inawacheleweshea stahiki zao zaidi ya miaka miwili.

“Mheshimiwa spika, serikali inasema kuhusu askari hawa ambao wamekuwa wakisumbuliwa kutolipwa stahiki zao baada ya kustaafu wakati polisi wanaotukamata na kutupiga wanalipwa mapema lakini wahalifu wote wanarundikwa magereza kwa hiyo hawa wanakuwa na kazi ngumu,” amesema Sugu.

Spika wa Bunge Job Ndugai amesema kuwa swali hilo licha ya kuwa ni refu lakini ameamua kuliacha lijibiwe kwani limeulizwa na mtu mzoefu kuliko maswali mengine yanayoulizwa kwa ubabaishaji.

Akijibu swali hilo na swali la msingi kutoka kwa mbuge wa Viti Maalum, Lucy Mlowe (Chadema), Naibu Waziri wa Fedha Dk. Ashatu Kijaji amesema Serikali inalipa mafao kwa wastaafu wote bila ya upendeleo na kuwa katika kipindi cha hivi karibuni, zililipwa jumla ya Sh 282 bilioni kwa wastaafu mbalimbali.

Naibu waziri amewaondoa hofu pia watumishi wote walioajiriwa katika miaka ya 1980 kupitia Serikali Kuu lakini wakati ule hapakuwa na makato ya mfuko wa kijamii.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!