Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Makao Makuu ya Mahakama Dodoma yaiva
Habari Mchanganyiko

Makao Makuu ya Mahakama Dodoma yaiva

Jaji Mkuu wa Tanzania Prof. Ibrahim Juma
Spread the love

JAJI Mkuu wa Tanzania Prof. Ibrahim Juma amezindua zoezi la upandaji miti katika kiwanja ambacho itajengwa Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania mkoani Dodoma. Anaripoti Dany Tibason … (endelea).

Akizindua zoezi la upandaji miti katika kiwanja hicho Jaji mkuu Prof. Juma amesema kuwa miti inazofaida nyingi katika maisha ya mwanadamu hivyo watumishi wa Mahakama Kuu Tanzania hawana budi kuitunza.

Amesema kiwanja hicho ambacho wamepatiwa na Manispaa ya Dodoma kwa ajili ya ujenzi wa Makao Makuu kitapendeza kama kitakuwa cha mafano katika suala la utunzaji wa mazingira.

Aidha amesema kuwa tafiti zinaonyesha kuwa mtu akipanda heka moja ya miti atakuwa ametoa hewa ya Oxygen kwa watu 18 kwa mwaka mzima.

Awali akisoma taarifa za kiwanja hicho Mkurugenzi Msaidizi wa Mipango Mahakama ya Tanzania, Erasmus Uisso amesema kuwa eneo hilo linaukubwa wa hekta 18.9 sawa na hekari 45.

Amesema katika eneo hilo wanatarajia kujengwa jengo la mahakama kuu, mahakama ya Rufani na masjala kuu na ujenzi unaanza ndani ya mwaka huu.

Amesema kuwa tayari wameshapatiwa hati ya eneo hilo ya miaka 99 na hivi sasa wapo katika mchakato wa kumtafuta mtaalam kwa ajili ya michoro pamoja na gharama za ujenzi.

“Tayari eneo hili tulishalifanyia utafiti wa kisayansi kubaini hali ya miamba pamoja na athari za matetemeko lakini wataalam wa masuala ya jiolojia walituambia kuwa hapa hakuna athari ya matetemeko hivyo tunaweza kuendelea na ujenzi kwani athari ya matetemeko ni kilomita 10 kutoka hapa,” amesema Uisso.

Aidha amesema kuwa pia katika eneo hilo kipo kiwacha chenye mita za mraba 9,000 kwa ajili ya ujenzi majengo ya mahakama kuu kanda ya kati, mahakama ya mkoa, Mahakama ya wilaya pamoja na mahakama ya mwanzo.

Naye Waziri wa Katiba na Sheria, Prof. Palamagamba Kabudi aliipongeza Mahakama Kuu ya Tanzania kwa kupata eneo hilo ambalo litajengwa makao makuu ya moja katia ya mihiri ya taifa.

Prof. Kabudi aliwataka kulitumia vizuri eneo na kujenga mahaka ambayo itakuwa ya mfano na inayoendana na makao makuu ya nchi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari Mchanganyiko

Chongolo aonya viongozi vijiji kutouza NIDA kwa wageni

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amewaonya viongozi wa...

error: Content is protected !!