Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge wa Chadema ang’ang’aniwa Polisi
Habari za SiasaTangulizi

Mbunge wa Chadema ang’ang’aniwa Polisi

Ester Bulaya na Halima Mdee walipowasili kituo Kikuu cha Polisi Dar es Salaam
Spread the love

MBUNGE wa Bunda Mjini, Ester Bulaya (Chadema) ameshikiliwa katika Kituo Kikuu cha Polisi Dar es Salaam (Central) kwa madai amebakishwa kwa ajili ya upelelezi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Bulaya aliripoti leo kituoni hapo baada ya kutakiwa kufanya hivyo, akiongozana na Viongozi wengine wa Chadema akiwemo Mwenyekiti, Freeman Mbowe ikiwa ni moja ya sharti la dhamana yao katika kesi inayowakabiri.

Katibu Mkuu wa Chadema, Vincent Mashinji amesema kuwa baada ya kuripoti kituoni hapo viongozi wote waliruhusiwa kuondoka lakini Bulaya alitakiwa kubaki kwa sababu ya upelelezi.

“Mbunge Bulaya amebaki mahabusu kwa sababu za kiupelelezi lakini tumeambiwa ataunganishwa katika shauri letu lililokuwa mahakamani Kisutu,” amesema Mashinji.

 

Hata hivyo ameeleza kuwa upelelezi utakapokamilika Bulaya atafikishwa mahakamani na kuunganishwa katika shauri la viongozi wengine ambao walishafikishwa mahakamani.

Kuripoti kwa viongozi hao ni moja ya sharti la dhamana katika kesi yao namba 112/2018 katika mahakama ya Kisutu Dar es Salaam.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!