Saturday , 4 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema waishtaki Serikali ya JPM Umoja wa Ulaya
Habari za SiasaTangulizi

Chadema waishtaki Serikali ya JPM Umoja wa Ulaya

Wabunge na Madiwani wa Chadema wakiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi wa Umoja wa Ulaya
Spread the love

WABUNGE na Madiwani wa Chama cha Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wameishitaki SErikali ya Tanzania kwa Umoja wa Ulaya juu ya hali ya kisiasa na kushinikiza kupatiwa dhamana viongozi wa chama hicho pamoja na kutahadhalisha usalama wa viongozi hao. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Viongozi hao waliongozwa na Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Godbles Lema, Peter Lijualikali, Mbunge wa Kilombero, Joseph Haule mbunge wa Mikumi. Wengine ni Boniface Jacob, Meya wa Ubungo, Patrick Ole Sosopi, Mwenyekiti wa Bavicha na wengine zaidi ya 30.

Viongozi wa chama hicho walikosa dhamana Machi 27, 2018 baada ya viongozi serikali kuzuia dhamana zao.
Lema aliyeongoza msafara huo alisema kuwa wataomba hati tahadhari kwenye ubalozi huo.

Amesema kuwa chama hicho kitawaomba ubalozi huo kusiishie tu kutoa matamko ya kupinga kinachoendelea nchini bali waende mbele zaidi na kwa kuchukua hatua stahiki.

Wabunge na Madiwani wa Chadema wakiwa katika mkutano na Ubalozi wa Umoja wa Ulaya
Wabunge na Madiwani wa Chadema wakiwa katika mkutano na Ubalozi wa Umoja wa Ulaya

Lema amesema kushikiliwa kwa viongozi wao kunatoa tafsiri kuwa chama chote kimefungwa gerezani licha kuwepo mkakati wa serikali kukifunga chama hicho.

Wakati Wabunge na Madiwani wa Chadema wakiwa Ubalozi wa Umoja wa Ulaya, kesi ya viongozi wao inaendelea Makahama ya Kisutu bila ya watuhumiwa kufikishwa mahakamani hapo.

Hakimu Mkazi, Wilbard Mashauri anasikiliza kesi hiyo na kutoa uamuzi wake juu ya dhamana yao. MwanaHALISI Online itawajuza kinachoendelea.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

error: Content is protected !!