Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe na wenzake wapata dhamana, kuachiwa Machi 3
Habari za Siasa

Mbowe na wenzake wapata dhamana, kuachiwa Machi 3

Spread the love

HAKIMU Mkazi wa Mahakama ya Kisutu, Wilbard Mashauri amewapa dhamana Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na viongozi wenzake watano bila ya kuwepo mahakamani. Anaripoti Jabir Idrissa … (endelea).

Hakimu Mashauri ametoa maamuzi hayo bila ya washitakiwa kuwepo mahakamani kutokana na kushindwa kuletwa kutoka gereza la Segerea walipokuwa mahabusu kwa madai gari liliharibika.

Mashauri amesema dhamana kwa watuhumiwa hao ipo wazi kwa masharti ya kusaini bondi ya Sh. 20 milioni kila mmoja pamoja na wadhamini wawili.

Viongozi hao waliokuwa mahabusu pamoja na Mbowe, ni Katibu Mkuu wa chama hicho, Vincent Mashinji, Naibu Katibu Mkuu Bara, John Mnyika, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Salum Mwalimu, Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa na Mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko.

Kabla ya kutoa uamuzi huo Hakimu Mashauri alipinga madai ya magereza ya kushindwa kuwaleta washtakiwa mahakamani kwa madai ya kuharibikiwa na gari, hivyo alilazimika kutoa uamuzi bila ya yao kuwepo na taratibu nyingine zitafuata.

Baada ya Hakimu Mashauri kusikiliza hoja za upande wa Serikali na utetezi katika kesi inayowakabili viongozi wa Chadema, amesema washtakiwa hao kuletwa mahakamani hapo Aprili 3, 2018 ili kutimiza masharti ya dhamana.

Written by
Jabir Idrissa

+255 774 226248

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Mwakyembe : Zanzibar waliongoza kutaka Serikali 2 za muungano

Spread the love  MWANASIASA mkongwe nchini, Dk. Harrison Mwakyembe, amesema mjadala wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

error: Content is protected !!