HAKIMU Mkazi wa Mahakama ya Kisutu, Wilbard Mashauri amewapa dhamana Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na viongozi wenzake watano bila ya kuwepo mahakamani. Anaripoti Jabir Idrissa … (endelea).
Hakimu Mashauri ametoa maamuzi hayo bila ya washitakiwa kuwepo mahakamani kutokana na kushindwa kuletwa kutoka gereza la Segerea walipokuwa mahabusu kwa madai gari liliharibika.
Mashauri amesema dhamana kwa watuhumiwa hao ipo wazi kwa masharti ya kusaini bondi ya Sh. 20 milioni kila mmoja pamoja na wadhamini wawili.
Viongozi hao waliokuwa mahabusu pamoja na Mbowe, ni Katibu Mkuu wa chama hicho, Vincent Mashinji, Naibu Katibu Mkuu Bara, John Mnyika, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Salum Mwalimu, Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa na Mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko.
Kabla ya kutoa uamuzi huo Hakimu Mashauri alipinga madai ya magereza ya kushindwa kuwaleta washtakiwa mahakamani kwa madai ya kuharibikiwa na gari, hivyo alilazimika kutoa uamuzi bila ya yao kuwepo na taratibu nyingine zitafuata.
Baada ya Hakimu Mashauri kusikiliza hoja za upande wa Serikali na utetezi katika kesi inayowakabili viongozi wa Chadema, amesema washtakiwa hao kuletwa mahakamani hapo Aprili 3, 2018 ili kutimiza masharti ya dhamana.
Leave a comment