Thursday , 18 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema waishtaki Serikali ya JPM Umoja wa Ulaya
Habari za SiasaTangulizi

Chadema waishtaki Serikali ya JPM Umoja wa Ulaya

Wabunge na Madiwani wa Chadema wakiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi wa Umoja wa Ulaya
Spread the love

WABUNGE na Madiwani wa Chama cha Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wameishitaki SErikali ya Tanzania kwa Umoja wa Ulaya juu ya hali ya kisiasa na kushinikiza kupatiwa dhamana viongozi wa chama hicho pamoja na kutahadhalisha usalama wa viongozi hao. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Viongozi hao waliongozwa na Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Godbles Lema, Peter Lijualikali, Mbunge wa Kilombero, Joseph Haule mbunge wa Mikumi. Wengine ni Boniface Jacob, Meya wa Ubungo, Patrick Ole Sosopi, Mwenyekiti wa Bavicha na wengine zaidi ya 30.

Viongozi wa chama hicho walikosa dhamana Machi 27, 2018 baada ya viongozi serikali kuzuia dhamana zao.
Lema aliyeongoza msafara huo alisema kuwa wataomba hati tahadhari kwenye ubalozi huo.

Amesema kuwa chama hicho kitawaomba ubalozi huo kusiishie tu kutoa matamko ya kupinga kinachoendelea nchini bali waende mbele zaidi na kwa kuchukua hatua stahiki.

Wabunge na Madiwani wa Chadema wakiwa katika mkutano na Ubalozi wa Umoja wa Ulaya
Wabunge na Madiwani wa Chadema wakiwa katika mkutano na Ubalozi wa Umoja wa Ulaya

Lema amesema kushikiliwa kwa viongozi wao kunatoa tafsiri kuwa chama chote kimefungwa gerezani licha kuwepo mkakati wa serikali kukifunga chama hicho.

Wakati Wabunge na Madiwani wa Chadema wakiwa Ubalozi wa Umoja wa Ulaya, kesi ya viongozi wao inaendelea Makahama ya Kisutu bila ya watuhumiwa kufikishwa mahakamani hapo.

Hakimu Mkazi, Wilbard Mashauri anasikiliza kesi hiyo na kutoa uamuzi wake juu ya dhamana yao. MwanaHALISI Online itawajuza kinachoendelea.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia kutunukiwa udaktari wa heshima Uturuki

Spread the loveBaraza la Chuo Kikuu cha Ankara, ambacho ni cha pili...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia atua Uturuki kwa ziara ya siku 5

Spread the loveRais Samia Suluhu Hassan leo Jumatano amewasili nchini Uturuki kwa...

Habari za SiasaTangulizi

Samia arejesha mikopo ya 10%, bilioni 227.96 zatengwa

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amerejesha utaratibu wa utoaji mikopo...

Habari za Siasa

Rais Samia amfariji mjane wa Musa Abdulrahman

Spread the loveRais Samia Suluhu Hassan leo Jumanne amempa pole Mwanakheri Mussa...

error: Content is protected !!