Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Nini kimetokea uchaguzi marudio udiwani
Habari za Siasa

Nini kimetokea uchaguzi marudio udiwani

Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji Semistocles Kaijage
Spread the love

KATIKA hali ya kawaida mtu anaweza kujiuliza nini kimetokea katika uchaguzi wa marudio katika kata 43 hapa nchini.
Siku za hivi karibuni kumekuwa na malalamiko mengi kutoka kwa wananchi wa kawaida kwamba maisha yamezidi kuwa magumu, anaandika Richard Makore.

Licha ya malalamiko hayo, lakini uchaguzi wa marudio uliofanyika jana Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimenyakua viti 42 na kuviacha mbali vyama vya upinzani.

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimejinyakulia kata moja licha ya wananchi kushuhudia umati mkubwa katika mikutano yao ya kampeni.

Bado kuna maswali mengi kuhusu matokeo hayo lakini ukweli ni kwamba yameishatangazwa.
Kata hizo 42 ni pamoja na Bomambuzi, Mnadani, Machame Magharibi, Weruweru, Kijichi, Mbweni, Saranga, Muungano na Mhongozi

Zingine ni pamoja na Majengo, Milongodi, Chipogoro, Muriet, Reli, Makiba, Moita, Musa, Maroroni, Mnacho, Kitwiru, Ambureni, Maloloni, Legeruki, Ngabobo, Nata na Siuyu.

Kata zingine ni pamoja ni Bonyokwa, Mhandu, Kimala, Senga, Kalulu, Kijima, Bukwimba, Lukumbile, Chanikanguo, Lunguza, Mamba, Nangwa, Kiloka, Ndalambo, Chikonji, Sumbawanga asilia na Ibhigi ambayo Chadema imeibuka na ushindi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

error: Content is protected !!