Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Nini kimetokea uchaguzi marudio udiwani
Habari za Siasa

Nini kimetokea uchaguzi marudio udiwani

Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji Semistocles Kaijage
Spread the love

KATIKA hali ya kawaida mtu anaweza kujiuliza nini kimetokea katika uchaguzi wa marudio katika kata 43 hapa nchini.
Siku za hivi karibuni kumekuwa na malalamiko mengi kutoka kwa wananchi wa kawaida kwamba maisha yamezidi kuwa magumu, anaandika Richard Makore.

Licha ya malalamiko hayo, lakini uchaguzi wa marudio uliofanyika jana Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimenyakua viti 42 na kuviacha mbali vyama vya upinzani.

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimejinyakulia kata moja licha ya wananchi kushuhudia umati mkubwa katika mikutano yao ya kampeni.

Bado kuna maswali mengi kuhusu matokeo hayo lakini ukweli ni kwamba yameishatangazwa.
Kata hizo 42 ni pamoja na Bomambuzi, Mnadani, Machame Magharibi, Weruweru, Kijichi, Mbweni, Saranga, Muungano na Mhongozi

Zingine ni pamoja na Majengo, Milongodi, Chipogoro, Muriet, Reli, Makiba, Moita, Musa, Maroroni, Mnacho, Kitwiru, Ambureni, Maloloni, Legeruki, Ngabobo, Nata na Siuyu.

Kata zingine ni pamoja ni Bonyokwa, Mhandu, Kimala, Senga, Kalulu, Kijima, Bukwimba, Lukumbile, Chanikanguo, Lunguza, Mamba, Nangwa, Kiloka, Ndalambo, Chikonji, Sumbawanga asilia na Ibhigi ambayo Chadema imeibuka na ushindi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!