Tuesday , 21 March 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Shambulio la makombora ya Urusi laua 53
Kimataifa

Shambulio la makombora ya Urusi laua 53

Spread the love

RAIA 53 wameuawa katika shambulio la kombora la Urusi katika kijiji kilichopo mashariki mwa Syria Al-Shafah, kundi la uangalizi linasema.

Shirika la uangalizi wa haki za binaadamu Syria lililo na makao yake Uingereza (SOHR) linasema 21 kati ya wanaoripotiwa kuuawa Jumapili ni watoto.

Kijiji hicho kipo Deir al-Zour, mojawapo ya majimbo ya mwisho ambako wangambo wa Islamic State wanendelea kudhibiti ardhi.

Awali SOHR lilisema watu 34 wameuawa katika makombora yaliolenga makaazi ya watu. “Idadi hiyo imeongezeka baada ya kuondolewa kifusi baada ya operesheni ya siku nzima ya uokozi,” Rami Abdel Rahman amesema.

Awali Urusi ilithibitisha kwamba walipuaji wasita wa mabomu ya masafa marefu walitekeleza mashambulio ya angani katika eneo hilo, lakini ikasema iliwalenga wanamgambo na ngome zao.

Urusi ni mshirika wa karibu wa rais wa Syria Bashar al-Assad katika vita vya muda mrefu vya kiraia nchini humo.

Mazungumzo ya amani yanayoungwamkono na Umoja wamataifa yanatarajiwa kuanza upya Geneva wiki ijayo, lakini awamu kadhaa za mazungumzo hayakufuwa dafu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Xi Jinping awasili Urusi, kufanya mazungumzo na Putin

Spread the love  RAIS wa uchini Xi Jinping amewasili sasa nchini Urusi,...

Kimataifa

Maandamano Kenya, Afrika Kusini yashika kasi, wapinzani wakishikiliwa

Spread the love  MAANDAMANO ya kupinga serikali zilizoko madarakani nchini Kenya na...

Kimataifa

Maandamano Afrika Kusini: Tanzania yatahadharisha raia wake

Spread the love  WAKATI maandamano yaliyoitishwa na Chama cha upinzani Afrika Kusini,...

Kimataifa

ICC yatoa hati ya kukamatwa kwa rais Vladmir Putin wa Urusi

Spread the love  MAHAKAMA ya Kimataifa ya Uhalifu wa kivita (ICC) imetoa...

error: Content is protected !!