Wednesday , 1 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa CHADEMA yatikiswa, wengine mbioni kung’oka
Habari za SiasaTangulizi

CHADEMA yatikiswa, wengine mbioni kung’oka

Wanachama wapya wa CCM waliojiunga na chama hicho wakitokea upinzani
Spread the love

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kinaweza kukimbiwa na viongozi wake wengine watatu, wakiwamo wabunge wawili wa majimbo, anaandika Mwandishi Wetu.

Taarifa kutoka ndani ya chama hicho na Ikulu jijini Dar es Salaam zinasema, mkakati mkali unasukwa wa kuwashawishi viongozi hao kukihama chama hicho na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Hata hivyo, mmoja wa viongozi anayeshawishiwa kuondoka amenukuliwa akisema, hajafikiria kufanya hivyo na kwamba hata ikimbidi kuondoka ndani ya Chadema, hatajiunga na CCM, bali atafanya shughuli zake binafsi.

Kupatikana kwa taarifa hizi kumekuja muda mchache baaada ya mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Pastrobas Katambi kujiunga na CCM leo Ikulu jijini Dar es Salaam.

Aidha, kupatikana kwa taarifa hizi kumekuja wiki tatu baada ya gazeti hili kuripoti kuwapo kwa mpango wa wabunge wa viongozi wa Chadema kukima chama hicho.

SOMA: Upinzani kupata pigo

1 Comment

  • Hakuna kitu apo, hata angehama Mbowe bado CDM Haitakufa watu wenye akili timamu ndi wanakuja kama Mhe Nyalandu, hatuangalii mtu na utashi wake kama patrobas ameshindwa kuitumikia nafasi yake njia iko wazi watakuja wengine.Hata kwenye kanisa watu wanaokoka na kurudi nyuma sembuse siasaAMERUDI KWENYE MATAPUTAPU HUYU, AMERUDIA MATAPISHI YAKE MWENYEWE

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!