Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Polisi wamng’ang’ania Kigaila, anyimwa dhamana
Habari za Siasa

Polisi wamng’ang’ania Kigaila, anyimwa dhamana

Benson Kigaila, Mkurugenzi wa Operesheni na Mafunzo wa Chadema
Spread the love

BENSON Kigaila, Mkurugenzi wa Operesheni na Mafunzo wa Chadema ametupwa rumande baada ya kukosa dhamana alipojisalimisha kuhojiwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, anaandika Faki Sosi.

Kigaila aliitwa kwa mahojiano kwa tuhuma za kutoa lugha za kichochezi katika mkutano wake na waandishi wa habari alioufanya Oktoba 12.

Frederick Kihwelo ambaye ni Mwanasheria wa Kigaila, amesema maamuzi juu ya dhamana ya mteja wake yataamuliwa kesho Jumanne.

”Polisi wamemhoji kwa masaa 3 kuanzia saa 7 hadi saa 10 na amehojiwa kwa makosa aliyoyafanya katika mkutano wake wa Oktoba 12 na wamekataa kutoa dhamana labda hadi kesho,” amesema Kihwelo.

KIhwelo ameongeza: ”Kimsingi makosa aanayotuhumiwa nayo yana dhamana, lakini wamesema wanaoweza kuamua ama kupata dhamana au kukosa hawapo ofisini.”

Mwanasheria huyo amesema katika mkutano huo Kigaila alizungumza mambo mengi ikiwamo kupigwa risasi kwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu na kutekwa kwa Ben Saanane.

Kaimu kamanda wa kanda hiyo, Benedict Kitalika amesema upepelezi kwa sehemu kubwa umekamilika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

error: Content is protected !!