Wednesday , 1 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Muswada wa kutambua madaktari wapitishwa
Habari Mchanganyiko

Muswada wa kutambua madaktari wapitishwa

Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
Spread the love

BUNGE limeridhia na kupitisha  muswada wa sheria ya madaktari, madaktari wa meno na wataalam wa afya shirikishi wa mwaka 2016, ambao utasimamia taaluma na maadili ya wanataaluma wa sekta ya afya ili kulinda usalama wa afya kwa Watanzania, anaandika Dany Tibason.

Pia serikali inatarajiwa kupeleka bungeni muswada  ambao utamlazimisha kila Mtanzania kuwa na bima ya afya kutokana na umuhimu wake katika suala la afya.

Akijibu hoja za wabunge waliochangia muswada huo, Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, amesema sababu ya kupelekwa kwa muswada huo ni  kutokana na kuwa na ongezeko la wataalam, ambapo hivi sasa Tanzania wanazalisha zaidi ya madaktari 1000 kwa mwaka na kuwa moja ya nchi zinazoongoza kwa  idadi kubwa ya watalaam hao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Habari Mchanganyiko

TMA yapongezwa kuimarisha ubora na usahihi wa taarifa za Hali ya Hewa

Spread the love  WAFANYAKAZI wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA),...

error: Content is protected !!