Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Muswada wa kutambua madaktari wapitishwa
Habari Mchanganyiko

Muswada wa kutambua madaktari wapitishwa

Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
Spread the love

BUNGE limeridhia na kupitisha  muswada wa sheria ya madaktari, madaktari wa meno na wataalam wa afya shirikishi wa mwaka 2016, ambao utasimamia taaluma na maadili ya wanataaluma wa sekta ya afya ili kulinda usalama wa afya kwa Watanzania, anaandika Dany Tibason.

Pia serikali inatarajiwa kupeleka bungeni muswada  ambao utamlazimisha kila Mtanzania kuwa na bima ya afya kutokana na umuhimu wake katika suala la afya.

Akijibu hoja za wabunge waliochangia muswada huo, Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, amesema sababu ya kupelekwa kwa muswada huo ni  kutokana na kuwa na ongezeko la wataalam, ambapo hivi sasa Tanzania wanazalisha zaidi ya madaktari 1000 kwa mwaka na kuwa moja ya nchi zinazoongoza kwa  idadi kubwa ya watalaam hao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!