Wednesday , 1 May 2024
Home Habari Mchanganyiko RPC Mambosasa atua Kanda Maalum Dar
Habari Mchanganyiko

RPC Mambosasa atua Kanda Maalum Dar

Lazaro Mambosasa, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam
Spread the love

MKUU wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP), Simon Sirro amemteu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma (SACP), Lazaro Mambosasa kuwa Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, anaandika Irene Emmanuel.

Kwa mujibu wa taarifa ya msemaji wa jeshi hilo, Barnabas Mwakalukwa, Sirro pia amemteua Kamishna Msaidizi wa Polisi (DCP), Juma Yusuf Ally kuwa Kaimu Kamishna wa Polisi Zanzibar.

Uteuzi wa makamanda hao unafuatia waliokuwapo kustaafu kwa mujibu wa sheria kwa kufikisha umri wa miaka 60.

Kabla ya uteuzi huo DCP Juma alikuwa ni Mkuu wa Utawala na Fedha Makao Makuu ya Polisi Zanzibar.

Sirro pia amewahamisha Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Temeke Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP), Gilles Bilabaye Mroto kuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma na Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Emmanuel Lukula kwenda kuwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Kipolisi Temeke.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Habari Mchanganyiko

TMA yapongezwa kuimarisha ubora na usahihi wa taarifa za Hali ya Hewa

Spread the love  WAFANYAKAZI wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA),...

error: Content is protected !!