Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Tundu Lissu aachiwa huru kwa dhamana
Habari za SiasaTangulizi

Tundu Lissu aachiwa huru kwa dhamana

Tundu Lissu, Mwanasheria Mkuu wa Chadema akitoka polisi baada ya kuachiwa kwa dhamana
Spread the love

TUNDU Lissu, Mwanasheria Mkuu wa Chadema, ameachiwa kwa dhamana ya Polisi kwa masharti ya kurudi tena polisi Jumatatu ya Agosti 28, mwaka huu, anaandika Hamisi Mguta.

Akizungumza na waandishi wa habari muda mfupi baada ya kutoka kituo cha Polisi Kanda ya Dar es Salaam, wakili wa Lissu, Peter Kibatala amesema tuhuma alizotakiwa kuziandikia maelezo ni za uchochezi na kutoa maneno ya kashfa.

“Kwa kuwa hatujakwenda mahakamani tutajua mbele ya safari lakini masharti ya dhamana anatakiwa kurudi tena tarehe 28,” amesema Kibatala.

Vionjo kuhusu Tundu 

Tarehe 18 Agosti alikutana na waandishi wa habari Hoteli ya Protea Courtyard, Upanga.

Tarehe 19 Agosti Serikali ikajibu kupitia Kaimu Msemaji wake, Zamaradi Kawawa.

Tarehe 22 Agosti alikamatwa akiwa anatoka Mahakama ya Kisutu.

Anapelekwa Central Polise Station. Baada ya maelezo huku Lissu akikataa kuandika maelezo, alilala huko.

Tarehe 23 Agosti anapelekwa nyumbani kwake kusachiwa.

Tarehe 24 Agosti anapelekwa kuandika dhamana ya maandishi ya Polisi.

Lissu ambaye wamili wake Peter Kibatala anasema anadaiwa kuwa amemkashifu rais kwa kuyasema makosa yake hadharani na amefana uchochezi kuhusu taarifa ya Bombadier kushikiliwa nchini Canada kwa deni, hajapelekwa mahakamani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaTangulizi

Mapya yaibuka wamasai waliohamishwa Ngorongoro kwenda Msomera

Spread the loveMAPYA yameibuka kuhusu zoezi la Serikali kuwahamisha kwa hiari wamasai...

Habari MchanganyikoTangulizi

Baba aomba msaada kuzika miili ya familia yake iliyofunga bila kula kuonana na Mungu

Spread the loveWAKATI Mamlaka nchini Kenya, ikiendelea kukabidhi miili ya watu waliofariki...

Habari za Siasa

Rais Samia ampongeza mpinzani aliyeshinda urais Senegal

Spread the loveRAIS wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amempongeza mwanasiasa wa...

error: Content is protected !!