TUNDU Lissu, Mwanasheria Mkuu wa Chadema, ameachiwa kwa dhamana ya Polisi kwa masharti ya kurudi tena polisi Jumatatu ya Agosti 28, mwaka huu, anaandika Hamisi Mguta.
Akizungumza na waandishi wa habari muda mfupi baada ya kutoka kituo cha Polisi Kanda ya Dar es Salaam, wakili wa Lissu, Peter Kibatala amesema tuhuma alizotakiwa kuziandikia maelezo ni za uchochezi na kutoa maneno ya kashfa.
“Kwa kuwa hatujakwenda mahakamani tutajua mbele ya safari lakini masharti ya dhamana anatakiwa kurudi tena tarehe 28,” amesema Kibatala.
Vionjo kuhusu Tundu
Tarehe 18 Agosti alikutana na waandishi wa habari Hoteli ya Protea Courtyard, Upanga.
Tarehe 19 Agosti Serikali ikajibu kupitia Kaimu Msemaji wake, Zamaradi Kawawa.
Tarehe 22 Agosti alikamatwa akiwa anatoka Mahakama ya Kisutu.
Anapelekwa Central Polise Station. Baada ya maelezo huku Lissu akikataa kuandika maelezo, alilala huko.
Tarehe 23 Agosti anapelekwa nyumbani kwake kusachiwa.
Tarehe 24 Agosti anapelekwa kuandika dhamana ya maandishi ya Polisi.
Lissu ambaye wamili wake Peter Kibatala anasema anadaiwa kuwa amemkashifu rais kwa kuyasema makosa yake hadharani na amefana uchochezi kuhusu taarifa ya Bombadier kushikiliwa nchini Canada kwa deni, hajapelekwa mahakamani.
Leave a comment