Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko RPC Mambosasa atua Kanda Maalum Dar
Habari Mchanganyiko

RPC Mambosasa atua Kanda Maalum Dar

Lazaro Mambosasa, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam
Spread the love

MKUU wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP), Simon Sirro amemteu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma (SACP), Lazaro Mambosasa kuwa Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, anaandika Irene Emmanuel.

Kwa mujibu wa taarifa ya msemaji wa jeshi hilo, Barnabas Mwakalukwa, Sirro pia amemteua Kamishna Msaidizi wa Polisi (DCP), Juma Yusuf Ally kuwa Kaimu Kamishna wa Polisi Zanzibar.

Uteuzi wa makamanda hao unafuatia waliokuwapo kustaafu kwa mujibu wa sheria kwa kufikisha umri wa miaka 60.

Kabla ya uteuzi huo DCP Juma alikuwa ni Mkuu wa Utawala na Fedha Makao Makuu ya Polisi Zanzibar.

Sirro pia amewahamisha Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Temeke Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP), Gilles Bilabaye Mroto kuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma na Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Emmanuel Lukula kwenda kuwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Kipolisi Temeke.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Watendaji Kata, Mitaa watakaoshindwa kusimamia usafi kukiona

Spread the love  WATENDAJI wa kata, mitaa na vitongoji na maofisa afya...

Habari Mchanganyiko

Mtia nia urais TLS kukata rufaa kupinga kuenguliwa

Spread the love  MTIA nia ya kugombea Urais wa Chama cha Mawakili...

Habari Mchanganyiko

NBC yazindua kampeni ya mkeka wa ushindi na ATM zake

Spread the loveBENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imetangaza uzinduzi wa kampeni...

Habari Mchanganyiko

Uholanzi wampongeza Rais Samia kuimarisha vyombo vya habari, demokrasia

Spread the love  UBALOZI wa Uholanzi nchini Tanzania, umempongeza Rais Samia Suluhu...

error: Content is protected !!