Thursday , 18 April 2024
Home Habari Mchanganyiko RPC Mambosasa atua Kanda Maalum Dar
Habari Mchanganyiko

RPC Mambosasa atua Kanda Maalum Dar

Lazaro Mambosasa, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam
Spread the love

MKUU wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP), Simon Sirro amemteu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma (SACP), Lazaro Mambosasa kuwa Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, anaandika Irene Emmanuel.

Kwa mujibu wa taarifa ya msemaji wa jeshi hilo, Barnabas Mwakalukwa, Sirro pia amemteua Kamishna Msaidizi wa Polisi (DCP), Juma Yusuf Ally kuwa Kaimu Kamishna wa Polisi Zanzibar.

Uteuzi wa makamanda hao unafuatia waliokuwapo kustaafu kwa mujibu wa sheria kwa kufikisha umri wa miaka 60.

Kabla ya uteuzi huo DCP Juma alikuwa ni Mkuu wa Utawala na Fedha Makao Makuu ya Polisi Zanzibar.

Sirro pia amewahamisha Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Temeke Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP), Gilles Bilabaye Mroto kuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma na Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Emmanuel Lukula kwenda kuwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Kipolisi Temeke.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

Habari Mchanganyiko

Serikali yatoa ajira watumishi 46,000, yatangaza utaratibu mpya kuajiri

Spread the loveSERIKALI imetangaza nafasi za ajira za watumishi wa umma 46,000...

Habari Mchanganyiko

Dereva ajali iliyoua wanafunzi Arusha afikishwa kortini, aomba apelekwe rumande

Spread the loveDEREVA aliyehusika katika ajali la basi la Shule ya Msingi...

Habari Mchanganyiko

Dereva ajali iliyoua wanafunzi Arusha afikishwa kortini, aomba apelekwe rumande

Spread the love  DEREVA aliyehusika katika ajali la basi la Shule ya...

error: Content is protected !!