Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema Dodoma wamtetea Lissu
Habari za Siasa

Chadema Dodoma wamtetea Lissu

Tundu Lissu, Mwanasheria Mkuu wa Chadema na Mbunge wa Singida, akiwasili katika Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kisutu
Spread the love

CHAMA Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kanda ya kati kimelaani kitendo cha jeshi la polisi nchini kumkamata mara kwa mara, mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema), anaandika Dany Tibason.

Akizungumza na MwanaHALISI Online, mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Kati, Alphonce Mbassa amesema kitendo cha polisi kumkamata mra kwa mara ni sawa na serikali kushindwa kufanya siasa za vyama vingi.

Amesema kwa kuwa kuna dalili hizo za kushindwa ni bora ipeleke muswada bungeni ili kuvifuta kabisa visiwepo.

“Kamwe siasa za chuki haziwezi kujenga nchi bali nchi inajengwa kwa siasa zenye hoja na tabia ya kuwakamata wapinzani mara kwa mara na kuwaweka ndani huku wanasiasa wa chama watawala wakiendelea kufanya ndivyo sivyo ni chuki za wazi,” amesema

Naye mwenyekiti wa baraza la vijana mastaafu mkoa wa Dodoma(Bavicha), Malambaya Manayanya amesema kwa sasa inaonekana wazi kuwa serikali inatumia jeshi la polisi kukandamiza upinzani.

Baadhi ya wakazi wa mji wa Dodoma pamoja na wanasiasa kutoka vyama vya siasa wamesema kwamba wanakerwa na vitendo vya jeshi la polisi kumkamata mara kwa mara Lissu.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wamesema kitendo cha kukamatwa mara kwa mara kinaonyesha kwamba mwanasiasa huyo ni tishio.

Wamesema kuendelea kumkamata ni sawa na kumpa umaarufu na kwamba jamii itaendelea kaumini maneno anayosema yana ukweli.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Samia awataka watanzania kudumisha muungano

Spread the loveRais wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania kuendeleza Muungano kwa...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

error: Content is protected !!