Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Polisi watinga nyumbani kwa Lissu kusaka barua ya Bombardier
Habari za SiasaTangulizi

Polisi watinga nyumbani kwa Lissu kusaka barua ya Bombardier

Ndege ya Bombardier aina ya Q400
Spread the love

MAOFISA wa jeshi la polisi wamekwenda nyumbani kwa mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), eneo la Tegeta jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kumpekua, anaandika Hellen Sisya.

Jana Lissu alikamatwa na polisi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kisutu na kupelekwa kituo kikuu cha polisi jijini Dar es Salaam.

Lissu anatuhumiwa kwa makosa mawili ambayo ni kumkashfu Rais John Magufuli ( kusema makosa ya Rais hadharani) na la pili ni uchochezi kwa kutoa taarifa kuhusu ndege inayoshikiliwa nje ya nchi.

Update

Makachero wa polisi wazingira kwa Lissu

Maaskari wa jeshi la polisi bado wametanda nyumbani kwa mbunge wa Singida mjini, Tundu Lissu, eneo la Tegeta jijini Dar es Salaam, wakiendelea na upekuzi ambao hata hivyo haujajulikana ni wa nini.

Kuna tetesi kwamba huenda makachero hao wanasaka nyaraka muhimu ama barua zinazohusu taarifa alizotoa Lissu kuhusu ndege ya Bombardier. kushikiliwa nje ya nchi.

Jana Lissu alikamatwa na kushikiliwa katika kituo kikuu cha polisi jijini Dar es Salaam na leo asubuhi kulikuwa na tetesi kwamba angepelekwa mahakamani , lakini baadaye ikajulikana hakupelekwa huko.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!