Tuesday , 30 May 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Polisi watinga nyumbani kwa Lissu kusaka barua ya Bombardier
Habari za SiasaTangulizi

Polisi watinga nyumbani kwa Lissu kusaka barua ya Bombardier

Ndege ya Bombardier aina ya Q400
Spread the love

MAOFISA wa jeshi la polisi wamekwenda nyumbani kwa mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), eneo la Tegeta jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kumpekua, anaandika Hellen Sisya.

Jana Lissu alikamatwa na polisi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kisutu na kupelekwa kituo kikuu cha polisi jijini Dar es Salaam.

Lissu anatuhumiwa kwa makosa mawili ambayo ni kumkashfu Rais John Magufuli ( kusema makosa ya Rais hadharani) na la pili ni uchochezi kwa kutoa taarifa kuhusu ndege inayoshikiliwa nje ya nchi.

Update

Makachero wa polisi wazingira kwa Lissu

Maaskari wa jeshi la polisi bado wametanda nyumbani kwa mbunge wa Singida mjini, Tundu Lissu, eneo la Tegeta jijini Dar es Salaam, wakiendelea na upekuzi ambao hata hivyo haujajulikana ni wa nini.

Kuna tetesi kwamba huenda makachero hao wanasaka nyaraka muhimu ama barua zinazohusu taarifa alizotoa Lissu kuhusu ndege ya Bombardier. kushikiliwa nje ya nchi.

Jana Lissu alikamatwa na kushikiliwa katika kituo kikuu cha polisi jijini Dar es Salaam na leo asubuhi kulikuwa na tetesi kwamba angepelekwa mahakamani , lakini baadaye ikajulikana hakupelekwa huko.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Uamuzi juu ya wakurugenzi kusimamia uchaguzi 13 Juni

Spread the love  MAHAKAMA ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACHPR), imepanga...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jeshi la Polisi kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika utafiti

Spread the love  JESHI la Polisi Nchini limesema kuwa katika kukabiliana na...

KimataifaTangulizi

Mtuhumiwa wa mauaji ya halaiki ya Rwanda akamatwa Afrika Kusini

Spread the love  MMOJA wa watuhumiwa wakuu wa mauaji ya Kimbari ya...

Habari za Siasa

Musoma Vijijini waomba ujenzi wa barabara uanze haraka

Spread the loveJIMBO la Musoma Vijijini, mkoani Mara, limeomba Serikali kuhakikisha ujenzi...

error: Content is protected !!