Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe amchongea Magufuli kwa wananchi
Habari za Siasa

Mbowe amchongea Magufuli kwa wananchi

Dk. John Pombe Magufuli, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) (Picha kubwa) na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Freeman Mbowe
Spread the love

FREEMAN Mbowe, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) amewataka watanzania kutokuogopa kumkosoa Rais John Magufuli pale anapokosea, anaandika Hellen Sisya.

Mbowe ameyasema hayo mapema leo hii katika hoteli ya Protea iliyopo Upanga jijini Dar es Salaam na kusisitiza kuwa endapo taifa litakuwa na watu waoga, basi kuna uwezekano wa taifa hilo kutawaliwa na dikteta.

“Anapostahili pongezi tumpe pongezi, anapostahili lawama tumpe lawama bila kuogopa. Tukiwa taifa la watu waoga Mwalimu Nyerere alituasa tutatawaliwa na dikteta “ amesema Mbowe.

Aidha, Mbowe amesisitiza kuwa watanzania wanapaswa kutambua kuwa kauli za Rais Magufuli sio sheria za nchi.

“Rais apongezwe pale anapofanya jambo jema. Lakini afanye jambo jema kwa misingi ya katiba, sheria pamoja na mikataba ambayo tunaingia. Tusiwe wepesi kumshangilia Rais kwa kila analolizungumza tukidhani ni jambo jema,” amesisitiza Mbowe

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Biteko aipongeza GGML kudhibiti vifo, majeruhi mahali pa kazi

Spread the loveNAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za Siasa

Askofu Shoo awataka ACT kupigania maslahi ya Taifa, wasikubali kuhongwa

Spread the loveALIYEKUWA Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri, Askofu...

Habari za Siasa

Biteko aagiza waajiri kudhibiti vifo mahali pa kazi

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

error: Content is protected !!