Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe amchongea Magufuli kwa wananchi
Habari za Siasa

Mbowe amchongea Magufuli kwa wananchi

Dk. John Pombe Magufuli, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) (Picha kubwa) na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Freeman Mbowe
Spread the love

FREEMAN Mbowe, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) amewataka watanzania kutokuogopa kumkosoa Rais John Magufuli pale anapokosea, anaandika Hellen Sisya.

Mbowe ameyasema hayo mapema leo hii katika hoteli ya Protea iliyopo Upanga jijini Dar es Salaam na kusisitiza kuwa endapo taifa litakuwa na watu waoga, basi kuna uwezekano wa taifa hilo kutawaliwa na dikteta.

“Anapostahili pongezi tumpe pongezi, anapostahili lawama tumpe lawama bila kuogopa. Tukiwa taifa la watu waoga Mwalimu Nyerere alituasa tutatawaliwa na dikteta “ amesema Mbowe.

Aidha, Mbowe amesisitiza kuwa watanzania wanapaswa kutambua kuwa kauli za Rais Magufuli sio sheria za nchi.

“Rais apongezwe pale anapofanya jambo jema. Lakini afanye jambo jema kwa misingi ya katiba, sheria pamoja na mikataba ambayo tunaingia. Tusiwe wepesi kumshangilia Rais kwa kila analolizungumza tukidhani ni jambo jema,” amesisitiza Mbowe

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!