NDEGE iliyonunuliwa na Rais John Magufuli, nchini Canada, aina ya Bombardier Q400, imekamatwa nchini humo na iko hatarini kuuzwa kwa mnada, anaandika Saed Kubenea.
Taarifa kutoka Montreal, Canada na wizara ya mambo ya nje jijini Dar es Salaam zinasema, kukamatwa kwa ndege hiyo, kunatokana na kampuni moja ya ujenzi ya nchi hiyo, kuidai serikali ya Tanzania kiasi cha dola za Marekani 38 milioni (zaidi ya Sh. 90 bilioni).
Gazeti hili imeona nyaraka kadhaa kutoka kampuni ambayo inadai serikali na ambayo imekamata ndege hiyo ili kufidia fedha zake.
Taarifa kamili juu ya kilichosababisha ndege hiyo kukamatwa, soma MwanaHALISI Jumatatu wiki ijayo.
Leave a comment