Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mdee aichana  bodi ya mikopo 
Habari za SiasaTangulizi

Mdee aichana  bodi ya mikopo 

Spread the love

Halima Mdee, Mbunge wa jimbo la kawe (Chadema) ameituhumu Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu nchini (HESLB) kwa kufanya ubaguzi wa elimu, anaandika Hellen Sisya

Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari, mbunge huyo amesema kuwa miongoni mwa sifa za waombaji ambazo zimeainishwa na bodi hiyo ni za kibaguzi ikiwemo kigezo namba 10 ambacho kinawataka  waombaji ambao wazazi wao ni viongozi wa umma  au kisiasa ambao wanatajwa na sheria ya maadili ya viongozi wa umma kutokuomba mikopo.

Kwa mujibu wa mbunge huyo, hata madiwani ambao hawana mshahara nao pia wanatajwa na sheria hiyo, hivyo kuwakataza watoto wao kuomba mikopo ni kuleta ubaguzi katika elimu.

“Kwa watu wa kawaida wakisikia watu wanaojaza fomu za maadili, wanajua labda ni ngazi za ubunge na mawaziri. Lakini pia hata katika hizo ngazi za ubunge, ama mawaziri, ama mkurugenzi,unamnyimanye mtu haki yake ya kikatiba, ya mtoto wake kupewa fursa ya elimu sambamba na mikopo, kwa kudhani kwamba huyu mtu mwenye nafasi hiyo, basi ana uwezo wa kulipa. Unajuaje kama analipia watoto 10  au 20  kwa mwaka?” alihoji Mdee

Kwa mujibu wa mbunge huyo, serikali inatumia hoja nyepesi na ambazo hazina mashiko kuleta ubaguzi katika sekta ya elimu,jambo ambalo wao kama chama watalikemea.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

error: Content is protected !!