Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge wa CCM amuangukia Waziri Mkuu Majaliwa
Habari za Siasa

Mbunge wa CCM amuangukia Waziri Mkuu Majaliwa

Mbunge wa viti maalum (CCM) Juliana Shonza
Spread the love

IMEELEZWA kuwa upungufu wa majengo ya kutolea tiba pamoja na vyumba vya kulaza wagonjwa katika hospitali ya wilaya ya Mbozi ni miongoni mwa mambo yanayochangia  wagonjwa kulala wawili hadi watatu katika kitanda kimoja, anaandika Mwandishi Wetu.

Kauli hiyo ilitolewa na Mbunge wa viti maalum (CCM) Juliana Shonza katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa mpira wa miguu uliopo mjini Vywawa ambapo alimuomba Waziri Mkuu kuwasaidia ili waondokane na shida hiyo.

Alisema hospitali hiyo imekuwa ikihudumia wakazi wa wilaya zaidi ya 300 na wengine wanatoka nchi jirani ya Zambi hivyo inakabiliwa na changamoto nyingi kutokana na kupokea wagonjwa wengi kuliko uwezo wake.

Naye Mbunge jimbo la Vwawa, Japhet Hasunga kupitia mkutano huo alimuomba Waziri Mkuu kutoa idhini ya ujenzi wa hospitali ya mkoa kujengwa eneo la Ilembo kwa kuwa ofisi za mkoa zimeanza kujengwa eneo la Selewa na Mbozi ijengwe Manispaa.

Alisema wakati wa kutafuta eneo la kujengwa ofisi za mkoa kulileta malumbano makubwa ambapo kila upande ulivutana, lakini baada ya serikali kupitisha eneo hilo la Selewa sasa tumetulia na sasa ombi letu wana Vywawa ni hospitali ya Mkoa ijengwe Ilembo.

Akijibu maombi hayo Waziri Majaliwa, alisema tayari serikali imetenga fedha kwa ajili ya kujenga hospitali ya wilaya kwa wilaya zote ambayo hazina hospitali na kuwa tatizo la ukosefu wa vyumba vya kulaza wagonjwa litapatiwa ufumbuzi kwa kuwa tayari serikali imeleta fedha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!