Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Watumiaji wa simu waondolewa hofu
Habari Mchanganyiko

Watumiaji wa simu waondolewa hofu

Watumiaji wa simu za mkononi
Spread the love

MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imewaondolea hofu watumiaji wa mitandao ya simu wanaotaka kutumia huduma ya laini moja kwa mitandao yote kuwa hatawakosa huduma zinazotolewa na makampuni ya simu, anaandika Mwandishi Wetu.

Kaimu Naibu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Tehama, Mhandisi Nehemia Mwenisongole, alisema hayo mjini hapa jana wakati akizungumza na waandishi wa habari.

Amesema huduma hiyo itakuwa ya hiari kwa watumiaji wa mitandao ya simu na itawasaidia kuondokana na kumiliki utitiri wa laini nyingi za simu na kutumia laini moja iliyobeba mitandao yote ya simu ambayo atahitaji kutumia.

“Ukiamua kuhamia kwenye mfumo huu wa kuunganishwa kutumia namba moja hakutakuwepo na madhara ya kuanza kuwaza kuwa wapo watu ambao nitawapoteza nikiingia huko,’’ alisema.

Aidha, amesema kuingia kwenye mfumo huo itasaidia kuondoa changamoto ya kukosekana kwa mtandao mahali mtumiaji atakapokuwa na kumsaidia kutumia mtandao mwingine utakaokua unapatikana eneo husika.

Amesema walianza kuingia kwenye mfumo huo wa mawasiliano kuanzia Machi mosi mwaka huu, ambapo alisema mchakato wa kuhamia mitandao mingine kwa kutumia namba moja hautazidi siku mbili.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

error: Content is protected !!