Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Watumiaji wa simu waondolewa hofu
Habari Mchanganyiko

Watumiaji wa simu waondolewa hofu

Watumiaji wa simu za mkononi
Spread the love

MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imewaondolea hofu watumiaji wa mitandao ya simu wanaotaka kutumia huduma ya laini moja kwa mitandao yote kuwa hatawakosa huduma zinazotolewa na makampuni ya simu, anaandika Mwandishi Wetu.

Kaimu Naibu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Tehama, Mhandisi Nehemia Mwenisongole, alisema hayo mjini hapa jana wakati akizungumza na waandishi wa habari.

Amesema huduma hiyo itakuwa ya hiari kwa watumiaji wa mitandao ya simu na itawasaidia kuondokana na kumiliki utitiri wa laini nyingi za simu na kutumia laini moja iliyobeba mitandao yote ya simu ambayo atahitaji kutumia.

“Ukiamua kuhamia kwenye mfumo huu wa kuunganishwa kutumia namba moja hakutakuwepo na madhara ya kuanza kuwaza kuwa wapo watu ambao nitawapoteza nikiingia huko,’’ alisema.

Aidha, amesema kuingia kwenye mfumo huo itasaidia kuondoa changamoto ya kukosekana kwa mtandao mahali mtumiaji atakapokuwa na kumsaidia kutumia mtandao mwingine utakaokua unapatikana eneo husika.

Amesema walianza kuingia kwenye mfumo huo wa mawasiliano kuanzia Machi mosi mwaka huu, ambapo alisema mchakato wa kuhamia mitandao mingine kwa kutumia namba moja hautazidi siku mbili.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Watendaji Kata, Mitaa watakaoshindwa kusimamia usafi kukiona

Spread the love  WATENDAJI wa kata, mitaa na vitongoji na maofisa afya...

Habari Mchanganyiko

Mtia nia urais TLS kukata rufaa kupinga kuenguliwa

Spread the love  MTIA nia ya kugombea Urais wa Chama cha Mawakili...

Habari Mchanganyiko

NBC yazindua kampeni ya mkeka wa ushindi na ATM zake

Spread the loveBENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imetangaza uzinduzi wa kampeni...

Habari Mchanganyiko

Uholanzi wampongeza Rais Samia kuimarisha vyombo vya habari, demokrasia

Spread the love  UBALOZI wa Uholanzi nchini Tanzania, umempongeza Rais Samia Suluhu...

error: Content is protected !!