Sunday , 28 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mongella atoa neno kwa wakazi wa Mwanza
Habari Mchanganyiko

Mongella atoa neno kwa wakazi wa Mwanza

John Mongella, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza
Spread the love

WANANCHI mkoani Mwanza wametakiwa kupenda kushiriki kikamilifu katika kupima Afya na kufanya usafi wa mazingira yanayowazunguka na wanayofanyia kazi ili kuweza kuondokana adha za kukumbwa na magonjwa yanayoweza kuepukika, anaadika Mwandishi Wetu.

Rai hiyo imetolewa na mkuu wa mkoa huo, John Mongella wakati akipongeza kamati ya ulinzi na usalama ya mkoani hapo pamoja na viongozi mbalimbali kwa kufanya usafi katika eneo la Soko la Kiloleli lililopo Manispaa ya Ilemela.

“Sisi vingozi na watumishi wa Umma ndio tuwe mstari wa mbele kupima afya na kuzingatia usafi wa mazingira ili kuweza kuwahamasisha wananchi ambao wamekuwa wakiogopa kupima afya zao kwa kuhofia kukutwa na mangonjwa makubwa, kitu ambacho kinahatarisha maisha ya wanajamii wengi.

Aidha, Mongella aliutaka uongozi wa soko la Kiloleli kugawa meza za wafanyabiashara zilizoachwa wazi kwa watu wanaohitaji ili kuweka mazingira katika hali ya usafi.

Naye mkuu wa vikosi vya Jeshi la Wananchi mkoa wa Mwanza, Kanali Albert Kitumbo alisema maadhimisho hayo yanaadhimishwa kwa kuwahamasisha wananchi kufanya usafi na kupima afya ili waweze kuishi kwa amani na kuzijenga familia nyingi.

Baadhi ya wakazi wa eneo hilo la Kiloleli ambalo maadhimisho siku ya Mashujaa kimkoa yalifanyika hapo, wamewataka wananchi wengine kupenda kujitokeza kushiriki kwenye shughuli za kijamii.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mvungi aendesha kikao kazi cha wataalam wa Regrow

Spread the love  MKURUGENZI wa Idara Sera na Mipango Wizara ya Maliasili...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

Polisi wakanusha kufanya uzembe ajali iliyouwa mwandishi Ayo Tv

Spread the loveJESHI la Polisi limekanusha tuhuma zilizoibuliwa dhidi yake  kwamba limekawia...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia kuzindua gazeti litakalotoa habari za wafanyakazi Tanzania

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), liko mbioni kufufua...

error: Content is protected !!