Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wachimbaji wadogo Sikonge wamwaga fedha serikalini  
Habari Mchanganyiko

Wachimbaji wadogo Sikonge wamwaga fedha serikalini  

Wachimbaji madini wadogo wadogo
Spread the love

KIKUNDI  cha wachimbaji wadogo kinachomiliki mgodi wa dhahabu wa Kapumpa uliopo tarafa ya Kitunda wilaya ya Sikonge Mkoani Tabora kimeongoza kwa kulipa mrabaha (royalty) wa zaidi ya Sh. 30 milioni serikalini kwa kipindi cha miezi mitatu kati ya migodi 617 yenye leseni, anaandika Mwandishi Wetu.

Kwa mujibu wa Kamishna Msaidizi wa Madini  wa Kanda hiyo,  Salim  Salim, kwa niaba ya Kamishna wa madini nchini, Benjamin Mchwampaka, katika taarifa yake  juu ya uchimbaji mdogo wa madini katika kanda hiyo, alisema leseni ya kikundi cha wachimbaji wadogo wa mgodi wa dhahabu wa Kapumpa  imeongoza kwa kulipa  Sh. 30.42 milioni kwa kipindi cha kati ya Mei na Julai, mwaka huu.

Aidha, leseni ya umoja wa wachimbaji wadogo wa dhahabu ya  wilayani Nzega Mkoa wa Tabora imefuatia kwa kulipa mrabaha wa Sh. 24.5 milioni, huku kikundi cha madini cha Tumaini kikishika nafasi ya tatu kwa kulipa Sh 22.4 milioni .

“Leseni ya mgodi wa Shukrani Chacha Chacha  wa Wilayani  Sikonge umeshika nafasi ya nne kwa kulipa mrabaha wa Sh. 14.9 milioni na mgodi wa Gregory Kibusi Gallid uliopo wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga wenyewe umelipa Sh.  3.99 milioni,” alisema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Gardner Habash wa Clouds Fm afariki dunia

Spread the loveALIYEKUWA mtangazaji wa kipindi cha Jahazi kinachorushwa na kituo cha...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

error: Content is protected !!