Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Ugonjwa wa ajabu watesa wanafunzi Tanga
Habari MchanganyikoTangulizi

Ugonjwa wa ajabu watesa wanafunzi Tanga

Spread the love

WANAFUNZI wanaosoma shule ya sekondari ya Kwamkabara kata ya Kwamkabara wilayani Muheza mkoani Tanga wamepatwa na ugonjwa wa ajabu unaosababisha kuanguka hovyo, anaandika Mwandishi Wetu.

Ugonjwa huo umesababisha wanafunzi 52 mpaka 70  wanaanguka baada ya kushikwa na ugonjwa waajabu wa kuanguka na kupiga kelele pamoja na kutokwa ute mdomoni kama wamepandisha mashetani.

Tukio hilo limetokea juzi katika shule hiyo ya sekondari ya kata ya Kwamkabara wilayani Muheza mkoani Tanga. Mkuu wa shule hiyo Getrude Moyo amethibitisha kuwapo tukio hilo la watoto kuanguka na kupiga kelele.

Akizungumza eneo la tukio Ofisa elimu wa shule za msingi wilayani Muheza, Julitha Akko amesema kuwa wanafunzi hao walishikwa na ugonjwa wa kuanguka na kupiga kelele kama wamepandisha mashetani.

Akko alisema kuwa mpaka sasa chanzo cha wanafunzi hao kuanguka na kupiga kelele bado hakijafahamika na wazazi kwa kushirikiana na walimu wa shule hiyo walifanya maombi ya kukemea mapepo  katika shule hiyo na baadae wanafunzi hao kuchukuliwa na kurudi nyumbani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!