Saturday , 4 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge wa CUF aburuzwa mahakamani
Habari za Siasa

Mbunge wa CUF aburuzwa mahakamani

Abdallah Mtolea, Mbunge wa Jimbo la Temeke (CUF)
Spread the love

ABDALLAH  Mtolea, Mbunge wa Jimbo la Temeke (CUF), amefikishwa  mahakamani kwa kosa la usalama barabarani, anaandika Hamisi Mguta.

Kamanda mkoa wa Polisi Temeke, Gilles Mroto,  akizungumza na MwanaHALISI Online kwa njia ya simu amesema, Mtolea alikamatwa jana na amefikishwa Mahakama ya Wilaya ya Temeke kwa makosa ya kuendesha gari lisilokatiwa bima na kushindwa kutii amri ya askari wa usalama barabarani.

Mtolea alikamatwa jana majira ya saa moja usiku na alikuwa akikabiliwa na makosa ya kuendesha gari bila ya bima kwa muda wake ulimalizika tangu Desemba 26  mwaka jana.

Kwa mujibu wa maelezo ya kamanda Mroto, Mtolea alikaidi agizo la askari wa usalama barabarani la kumtaka asimame badala yake alikaidi na kuwasha gari na kuondoka.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

error: Content is protected !!