Monday , 5 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge wa CUF aburuzwa mahakamani
Habari za Siasa

Mbunge wa CUF aburuzwa mahakamani

Abdallah Mtolea, Mbunge wa Jimbo la Temeke (CUF)
Spread the love

ABDALLAH  Mtolea, Mbunge wa Jimbo la Temeke (CUF), amefikishwa  mahakamani kwa kosa la usalama barabarani, anaandika Hamisi Mguta.

Kamanda mkoa wa Polisi Temeke, Gilles Mroto,  akizungumza na MwanaHALISI Online kwa njia ya simu amesema, Mtolea alikamatwa jana na amefikishwa Mahakama ya Wilaya ya Temeke kwa makosa ya kuendesha gari lisilokatiwa bima na kushindwa kutii amri ya askari wa usalama barabarani.

Mtolea alikamatwa jana majira ya saa moja usiku na alikuwa akikabiliwa na makosa ya kuendesha gari bila ya bima kwa muda wake ulimalizika tangu Desemba 26  mwaka jana.

Kwa mujibu wa maelezo ya kamanda Mroto, Mtolea alikaidi agizo la askari wa usalama barabarani la kumtaka asimame badala yake alikaidi na kuwasha gari na kuondoka.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Mwinyi azindua Kamati ya Maridhiano Visiwani

Spread the love  RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk. Hussein...

error: Content is protected !!