Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge wa CUF aburuzwa mahakamani
Habari za Siasa

Mbunge wa CUF aburuzwa mahakamani

Abdallah Mtolea, Mbunge wa Jimbo la Temeke (CUF)
Spread the love

ABDALLAH  Mtolea, Mbunge wa Jimbo la Temeke (CUF), amefikishwa  mahakamani kwa kosa la usalama barabarani, anaandika Hamisi Mguta.

Kamanda mkoa wa Polisi Temeke, Gilles Mroto,  akizungumza na MwanaHALISI Online kwa njia ya simu amesema, Mtolea alikamatwa jana na amefikishwa Mahakama ya Wilaya ya Temeke kwa makosa ya kuendesha gari lisilokatiwa bima na kushindwa kutii amri ya askari wa usalama barabarani.

Mtolea alikamatwa jana majira ya saa moja usiku na alikuwa akikabiliwa na makosa ya kuendesha gari bila ya bima kwa muda wake ulimalizika tangu Desemba 26  mwaka jana.

Kwa mujibu wa maelezo ya kamanda Mroto, Mtolea alikaidi agizo la askari wa usalama barabarani la kumtaka asimame badala yake alikaidi na kuwasha gari na kuondoka.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Mwakyembe : Zanzibar waliongoza kutaka Serikali 2 za muungano

Spread the love  MWANASIASA mkongwe nchini, Dk. Harrison Mwakyembe, amesema mjadala wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

error: Content is protected !!