Sunday , 28 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Muuguzi aliyebaka kutimuliwa  kazi 
Habari Mchanganyiko

Muuguzi aliyebaka kutimuliwa  kazi 

Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
Spread the love

SAKATA la  Muuguzi anayedaiwa kumbaka binti mwenye miaka 18 limeingia katika sura mpya, baada ya serikali kuingilia kati na kuomba Baraza la Wauguzi Tanzania kumsimamisha kazi mtumishi huyo, anaandika Hamisi Mguta.

Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imeomba kusitishwa kwa muda leseni ya uuguzi na ukunga ya Damian Mguya baada ya kumbaka binti wa miaka 18.

Nsachris Mwamwacha, Msemaji wa Idara kuu ya Afya amesema kupitia taarifa yake kuwa muuguzi huyo alimbaka binti huyo baada ya kumdunga sindano ya usingizi.

“Uamuzi huo wa serikali umetokana na tuhuma za uvunjifu wa maadili ya taaluma kwa mujibu wa kifungu 13 (2) (c) na (d) ya (The Nursing and Midwifery act 2010),” amesema Mwamwacha.

Mguya (26) alishikiliwa na polisi wilayani Igunga, Tabora baada ya kufanya tukio hilo ambapo kwa mujibu wa Kamishna Wilbroad Mutafungwa, Kamanda wa Polisi mkoni humo alihojiwa na atafikishwa Mahakamani uchunguzi utakapokamilika.

Imeelezwa kuwa siku ya tukio msichana huyo alifika kwenye Zahanati kwa ajili ya kumuuguza Mama yake mzazi, ndipo muuguzi huyo alipotumia nafasi hiyo kumchoma sindano ya usingizi kisha kumbaka.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mvungi aendesha kikao kazi cha wataalam wa Regrow

Spread the love  MKURUGENZI wa Idara Sera na Mipango Wizara ya Maliasili...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

Polisi wakanusha kufanya uzembe ajali iliyouwa mwandishi Ayo Tv

Spread the loveJESHI la Polisi limekanusha tuhuma zilizoibuliwa dhidi yake  kwamba limekawia...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia kuzindua gazeti litakalotoa habari za wafanyakazi Tanzania

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), liko mbioni kufufua...

error: Content is protected !!