Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Muuguzi aliyebaka kutimuliwa  kazi 
Habari Mchanganyiko

Muuguzi aliyebaka kutimuliwa  kazi 

Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
Spread the love

SAKATA la  Muuguzi anayedaiwa kumbaka binti mwenye miaka 18 limeingia katika sura mpya, baada ya serikali kuingilia kati na kuomba Baraza la Wauguzi Tanzania kumsimamisha kazi mtumishi huyo, anaandika Hamisi Mguta.

Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imeomba kusitishwa kwa muda leseni ya uuguzi na ukunga ya Damian Mguya baada ya kumbaka binti wa miaka 18.

Nsachris Mwamwacha, Msemaji wa Idara kuu ya Afya amesema kupitia taarifa yake kuwa muuguzi huyo alimbaka binti huyo baada ya kumdunga sindano ya usingizi.

“Uamuzi huo wa serikali umetokana na tuhuma za uvunjifu wa maadili ya taaluma kwa mujibu wa kifungu 13 (2) (c) na (d) ya (The Nursing and Midwifery act 2010),” amesema Mwamwacha.

Mguya (26) alishikiliwa na polisi wilayani Igunga, Tabora baada ya kufanya tukio hilo ambapo kwa mujibu wa Kamishna Wilbroad Mutafungwa, Kamanda wa Polisi mkoni humo alihojiwa na atafikishwa Mahakamani uchunguzi utakapokamilika.

Imeelezwa kuwa siku ya tukio msichana huyo alifika kwenye Zahanati kwa ajili ya kumuuguza Mama yake mzazi, ndipo muuguzi huyo alipotumia nafasi hiyo kumchoma sindano ya usingizi kisha kumbaka.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!