Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Kesi ya Manji yapigwa kalenda
Habari Mchanganyiko

Kesi ya Manji yapigwa kalenda

Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam imeahirisha kesi inayomkabili Yusuph Manji, Mwenyekiti wa Klabu ya Yanga, anaandika Hamisi Mguta.

Manji ambaye pia ni mfanyabiashara maarufu hapa nchini anakabiliwa na kesi ya kukutwa na sare za Jeshi la Wananchi wa Tanzania pamoja na mihuri kadhaa ya jeshi hilo kinyume cha sheria.

Kesi hiyo iliyopangwa kusikilizwa leo, haikusikilizwa kutokana na mahakama kuambiwa kwamba upelelezi wake haujakamilika.

Aidha, jana mtuhumiwa huyo alikwama kufika mahakamani hapo kwa madai kwamba ni mgonjwa na anadaiwa kupelekwa Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Madai hayo ya Manji kuumwa yametolewa leo katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam na wakili wake.

Kesi ya mfanyabiashara huyo imepangwa kusikilizwa Agost 4, mwaka huu.

Manji alisomewa mashtaka saba Julai 5 mwaka huu akiwa amelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na watuhumiwa wenzake, kwa makosa ya uhujumu uchumi, kukutwa na mihuri miwili ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NMB yakabidhi vifaa vya ujenzi, samani kwa shule ya msingi Sinyaulime, Chuo cha FDC Morogoro

Spread the loveBENKI ya NMB imekabidhi vifaa vya ujenzi kwa shule ya...

Habari Mchanganyiko

NMB Bonge la Mpango – ‘Moto Uleule’ yazinduliwa, Milioni 180…

Spread the loveMSIMU wa tatu wa Kampeni ya kuhamasisha utamaduni wa Kuweka...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo...

Habari Mchanganyiko

STAMICO yasaini mkataba wa bilioni 55.2 kuchoronga miamba GGML

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limezidi kufanya vizuri katika...

error: Content is protected !!