Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Kampuni ya Chai Kagera yakumbwa na ukata
Habari Mchanganyiko

Kampuni ya Chai Kagera yakumbwa na ukata

Shamba la chai Kagera
Spread the love

WIZARA ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, imetaja kuwa ucheleweshaji wa malipo ya wakulima na wafanyakazi katika kiwanda cha chai cha Maruku mkoani Kagera ulianza Septemba, 2011 kutokana na uwezo mdogo wa kifedha wa Kagera Tea Company Ltd, anaandika Dany Tibason.

Naibu Waziri wa Wizara hiyo, William Ole Nasha alitoa kauli hiyo bungeni wakati akijibu swali la Mbunge wa Bukoba (CCM), Jasson Rweikiza.

Rweikiza alitaka kujua ni kwanini serikali haichukui hatua ya kuwasaidia wakulima na wafanyakazi ili wapate haki yao ambayo wamekuwa wakiitafuta kwa muda mrefu bila mafanikio.

“Kampuni ya chai ya Maruku imekuwa sugu kwa kutowalipa wakulima wanaoiuzia chai pamoja na kutowalipa wafanyakazi wake wenyewe,” amesema mbunge huyo.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri amesema kutolipwa kwa wakulima na wafanyakazi hao kulitokana na uwezo mdogo wa kifedha wa Kagera Tea Ltd iliyowekwa na Spearshield Africa Company Ltd anayemiliki kiwanda cha chai cha Maruku.

Alibainisha kuwa anamiliki kwa asilimia 75 katika kusimamia uendeshaji wake ikiwemo ununuzi wa majani mabichi ya chai kutoka kwa wakulima wadogo huku wakulima hao wakimiliki asilimia 25 walizopewa na serikali kufuatia kiwanda hicho kubinafsishwa kwa Spearshield Africa Company Ltd toka kwa mamlaka ya chai Tanzania waliokuwa wanamiliki kiwanda hicho.

Alitaja sababu nyingine kuwa ni tija ndogo ya majani ya chai ikilinganishwa na gharama za uzalishaji lakini akasema serikali kupitia uongozi wa mkoa wa Kagera, Bodi ya Chai Tanzania na wakala wa wakulima wadogo wa chai Tanzania kwa nyakati tofauti walikutana na mwekezaji huyo kumwelekeza atekeleze wajibu wake wa kulipa wakulima na wafanyakazi.

Kwa mujibu wa Ole Nasha, kufuatia mikutano hiyo mwekezaji ametafuta fedha na kulipa madeni mbalimbali ikiwemo malimbikizo yote ya nyuma hadi mwezi Oktoba 2016 na ameahidi kulipa madeni ya Novemba Desemba 2016 ndani ya Januari 2017.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mvungi aendesha kikao kazi cha wataalam wa Regrow

Spread the love  MKURUGENZI wa Idara Sera na Mipango Wizara ya Maliasili...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

Polisi wakanusha kufanya uzembe ajali iliyouwa mwandishi Ayo Tv

Spread the loveJESHI la Polisi limekanusha tuhuma zilizoibuliwa dhidi yake  kwamba limekawia...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia kuzindua gazeti litakalotoa habari za wafanyakazi Tanzania

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), liko mbioni kufufua...

error: Content is protected !!