Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Tanroads yatenga bil 3 kujenga madaraja Masasi
Habari Mchanganyiko

Tanroads yatenga bil 3 kujenga madaraja Masasi

Moja ya barabara za Masasi zinavyoonekana wakati wa mvua
Spread the love

WAKALA wa Barabara Tanzania (Tanroads), umekubali kutenga fedha kiasi cha Sh. 3 bilioni kwa ajili madaraja ya Halmashauri ya wilayani Masasi katika bajeti ya mwaka 2017/18, bunge lilielezwa, anaandika Dany Tibason.

Kauli hiyo ilitolewa jana bungeni Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Seleman Jafo alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Lulindi (CCM), Jerome Bwanausi.

Bwanausi alitaka kujua ni lini madaraja ya Shaurimoyo, Nakalolo na Miesi yatajengwa ili kuwasaidia wananchi wa maeneo hayo ambao wamekuwa na adha kubwa ya usafiri.

Akijibu swali hilo, Jafo amesema kutokana na ufinyu wa bajeti ya Halmashauri hiyo, Wakala huo chini ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano imekubali kutenga fedha hizo kwa ajili ya ujenzi ambao utaanza mara moja baada ya fedha kupatikana.

Amesema Halmashauri hiyo kwa msaada wa Tanroads imekamilisha usanifu wa madaraja yanayohitajika kujengwa katika mito ya Mpindimbi-Shaurimoyo na Kanyimbi-Nakololo ambayo kwa pamoja yatagharimu Sh. 3 bilioni.

Jafo akijibu swali hilo alisema tathmini imeshafanyika tayari na ujenzi utaanza baada ya Bajeti hiyo kupitishwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!