Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kimbisa, Maghembe kuwania ubunge wa Afrika Mashariki
Habari za Siasa

Kimbisa, Maghembe kuwania ubunge wa Afrika Mashariki

Katibu wa itikadi na uenezi wa Chama Cha Mapinduzi CCM , Humphrey Polepole
Spread the love

CHAMA Cha Mapinzuzi CCM leo kimeteua wanachama 12 wa Tanzania Bara na Visiwani watakaoomba ridhaa kwa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa wajumbe wa Bunge la Afrika Mashariki, anaandika Hamisi Mguta.

Majina hayo yametangazwa kupitia kwa Humphrey Polepole, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, katika ofisi  ndogo Lumumba.

Polepole amesema chama hicho kimezingatia suala ya jinsia ambapo kuna idadi sawa ya wagombea wanaume na wagombea wanawake, huku pia suala la maadili likizingatiwa kwa kina.

Kwa Tanzania Bara kimeteua wajumbe nane ambao ni Zainab Rashid Mfaume Kawawa, Happiness Lugiko, Fancy Haji Nkuhi na Happiness Mgalula kwa upande wa wanawake.

Huku upande wa wanaume Dk. Ngwaru Jumanne Maghembe, Adam Omari Kimbisa, Anamringi Issay Macha na Charles Makongoro Nyerere.

Amesema wajumbe hao wote wamewachuja na kubaini kwamba wanazo sifa za kitaaluma hivyo wanachama wa chama hicho wasiwe na wasiwasi.

“Tumeyapitisha kwenye tanuli la kuwatazama uadilifu wao, uchapakazi wao, kwa sababu maadili ni jambo muhimu sana, ” amesema Polepole.

Kwa upande wa Visiwani kimewachagua Maryam Ussi Yahya, Rabia Abdallah Hamad kwa wanawake na wanaume ni Abdallah Hasnu Makame na Mohamed Yussuf Nuh.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

error: Content is protected !!