Thursday , 23 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mahakama Kuu yamtoa Lijualikali gerezani
Habari za SiasaTangulizi

Mahakama Kuu yamtoa Lijualikali gerezani

Peter Lijualikali, Mbunge wa Kilombelo (kushoto) ajidaliana na polisi wakati wa kesi yake
Spread the love

PETER Lijualikali (30), Mbunge wa Kilombero kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) yupo huru. Amevuka vinzingiti dhidi ya haki. Ameshinda kesi ya rufaa ya jinai Na. 60 ya mwaka huu katika Mahakama Kuu, anaandika Pendo Omary.

Mbali na Lijuakali lakini dereva wake, Stephano Mgata (35), aliyehukumiwa kifungo cha nje cha miezi sita, naye yupo huru.

Uamuzi huo umetolewa leo mbele ya Jaji Ama- Isaria Munisi baada ya kupitia sababu za kupinga mbunge huyo kutiwa hatiani na kuhukumuwa kifungo cha miezi sita jela.

Lijualikali na Mgata waliwakilishwa mahakamani na mawakili Tundu Lissu na Frederick Kihwelu huku upande wa Jamhuri ukiwakilishwa na wakili wa serikali, Faraja Nchimbi.

Kihwelu ameuambia MwanaHALISI Online mchana huu kwamba: “Sababu ya Lijualikali kushinda kesi ni hati ya mashtaka dhidi ya Lijualikali kutofautiana na maelezo ya mashtataka yaliyotolewa dhidi yake.

“Mh. Jaji alijielekeza kuangalia hati ya mashtaka. Ilikuwa na mapungufu mengi. Kubwa ni kwamba ilitofautiana na maelezo yalitolewa ya mashtaka. Hili ni takwa likisheria lazima hati ya mashtaka na maelezo vifanane. Hivyo ameamua kufuta hukumu,” anasema Kihwelu.

Hukumu dhidi ya Lijualikali ilitolewa Januari 11, 2017 na Mahakama ya Wilaya ya Kilombero, Morogoro chini ya Hakimu Mkazi, Timothy Lyon, kwa kosa la “kufanya fujo na kusababisha taharuki” huku Stephano Mgata (35) ambaye ni dereva wake akiwa mshitakiwa wa pili akifugwa kifungo cha miezi sita nje.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

error: Content is protected !!