Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mahakama Kuu yamtoa Lijualikali gerezani
Habari za SiasaTangulizi

Mahakama Kuu yamtoa Lijualikali gerezani

Peter Lijualikali, Mbunge wa Kilombelo (kushoto) ajidaliana na polisi wakati wa kesi yake
Spread the love

PETER Lijualikali (30), Mbunge wa Kilombero kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) yupo huru. Amevuka vinzingiti dhidi ya haki. Ameshinda kesi ya rufaa ya jinai Na. 60 ya mwaka huu katika Mahakama Kuu, anaandika Pendo Omary.

Mbali na Lijuakali lakini dereva wake, Stephano Mgata (35), aliyehukumiwa kifungo cha nje cha miezi sita, naye yupo huru.

Uamuzi huo umetolewa leo mbele ya Jaji Ama- Isaria Munisi baada ya kupitia sababu za kupinga mbunge huyo kutiwa hatiani na kuhukumuwa kifungo cha miezi sita jela.

Lijualikali na Mgata waliwakilishwa mahakamani na mawakili Tundu Lissu na Frederick Kihwelu huku upande wa Jamhuri ukiwakilishwa na wakili wa serikali, Faraja Nchimbi.

Kihwelu ameuambia MwanaHALISI Online mchana huu kwamba: “Sababu ya Lijualikali kushinda kesi ni hati ya mashtaka dhidi ya Lijualikali kutofautiana na maelezo ya mashtataka yaliyotolewa dhidi yake.

“Mh. Jaji alijielekeza kuangalia hati ya mashtaka. Ilikuwa na mapungufu mengi. Kubwa ni kwamba ilitofautiana na maelezo yalitolewa ya mashtaka. Hili ni takwa likisheria lazima hati ya mashtaka na maelezo vifanane. Hivyo ameamua kufuta hukumu,” anasema Kihwelu.

Hukumu dhidi ya Lijualikali ilitolewa Januari 11, 2017 na Mahakama ya Wilaya ya Kilombero, Morogoro chini ya Hakimu Mkazi, Timothy Lyon, kwa kosa la “kufanya fujo na kusababisha taharuki” huku Stephano Mgata (35) ambaye ni dereva wake akiwa mshitakiwa wa pili akifugwa kifungo cha miezi sita nje.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Mwakyembe : Zanzibar waliongoza kutaka Serikali 2 za muungano

Spread the love  MWANASIASA mkongwe nchini, Dk. Harrison Mwakyembe, amesema mjadala wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

error: Content is protected !!