Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kimbisa, Maghembe kuwania ubunge wa Afrika Mashariki
Habari za Siasa

Kimbisa, Maghembe kuwania ubunge wa Afrika Mashariki

Katibu wa itikadi na uenezi wa Chama Cha Mapinduzi CCM , Humphrey Polepole
Spread the love

CHAMA Cha Mapinzuzi CCM leo kimeteua wanachama 12 wa Tanzania Bara na Visiwani watakaoomba ridhaa kwa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa wajumbe wa Bunge la Afrika Mashariki, anaandika Hamisi Mguta.

Majina hayo yametangazwa kupitia kwa Humphrey Polepole, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, katika ofisi  ndogo Lumumba.

Polepole amesema chama hicho kimezingatia suala ya jinsia ambapo kuna idadi sawa ya wagombea wanaume na wagombea wanawake, huku pia suala la maadili likizingatiwa kwa kina.

Kwa Tanzania Bara kimeteua wajumbe nane ambao ni Zainab Rashid Mfaume Kawawa, Happiness Lugiko, Fancy Haji Nkuhi na Happiness Mgalula kwa upande wa wanawake.

Huku upande wa wanaume Dk. Ngwaru Jumanne Maghembe, Adam Omari Kimbisa, Anamringi Issay Macha na Charles Makongoro Nyerere.

Amesema wajumbe hao wote wamewachuja na kubaini kwamba wanazo sifa za kitaaluma hivyo wanachama wa chama hicho wasiwe na wasiwasi.

“Tumeyapitisha kwenye tanuli la kuwatazama uadilifu wao, uchapakazi wao, kwa sababu maadili ni jambo muhimu sana, ” amesema Polepole.

Kwa upande wa Visiwani kimewachagua Maryam Ussi Yahya, Rabia Abdallah Hamad kwa wanawake na wanaume ni Abdallah Hasnu Makame na Mohamed Yussuf Nuh.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!