Monday , 5 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Kimbisa, Maghembe kuwania ubunge wa Afrika Mashariki
Habari za Siasa

Kimbisa, Maghembe kuwania ubunge wa Afrika Mashariki

Katibu wa itikadi na uenezi wa Chama Cha Mapinduzi CCM , Humphrey Polepole
Spread the love

CHAMA Cha Mapinzuzi CCM leo kimeteua wanachama 12 wa Tanzania Bara na Visiwani watakaoomba ridhaa kwa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa wajumbe wa Bunge la Afrika Mashariki, anaandika Hamisi Mguta.

Majina hayo yametangazwa kupitia kwa Humphrey Polepole, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, katika ofisi  ndogo Lumumba.

Polepole amesema chama hicho kimezingatia suala ya jinsia ambapo kuna idadi sawa ya wagombea wanaume na wagombea wanawake, huku pia suala la maadili likizingatiwa kwa kina.

Kwa Tanzania Bara kimeteua wajumbe nane ambao ni Zainab Rashid Mfaume Kawawa, Happiness Lugiko, Fancy Haji Nkuhi na Happiness Mgalula kwa upande wa wanawake.

Huku upande wa wanaume Dk. Ngwaru Jumanne Maghembe, Adam Omari Kimbisa, Anamringi Issay Macha na Charles Makongoro Nyerere.

Amesema wajumbe hao wote wamewachuja na kubaini kwamba wanazo sifa za kitaaluma hivyo wanachama wa chama hicho wasiwe na wasiwasi.

“Tumeyapitisha kwenye tanuli la kuwatazama uadilifu wao, uchapakazi wao, kwa sababu maadili ni jambo muhimu sana, ” amesema Polepole.

Kwa upande wa Visiwani kimewachagua Maryam Ussi Yahya, Rabia Abdallah Hamad kwa wanawake na wanaume ni Abdallah Hasnu Makame na Mohamed Yussuf Nuh.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Mwinyi azindua Kamati ya Maridhiano Visiwani

Spread the love  RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk. Hussein...

error: Content is protected !!