Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Gwajima akamatwa, Kamanda Sirro ‘amkana’
Habari MchanganyikoTangulizi

Gwajima akamatwa, Kamanda Sirro ‘amkana’

Josephat Gwajima, Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima
Spread the love

MUDA mchache baada ya kusambaa kwa taarifa katika mitandao ya kijamii juu ya kukamatwa kwa Askofu Josephat Gwajima wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Simon Sirro Kamishna wa Polisi Kanda Malum ya Dar es Salaam amesema bado hana taarifa juu ya suala hilo, anaandika Charles William.

Mapema leo mchana zilisambaa taarifa katika mitandao ya kijamii kuwa Jeshi la Polisi jijini Dar limemkamata Askofu Gwajima nyumbani kwake na kumfanyia upekuzi na kwamba baada ya kumpekua limempeleka Kituo cha Polisi cha Kati.

Hata hivyo, taarifa hiyo katika mitandao ya kijamii haikufafanua zaidi kuwa, Askofu Gwajima amekamatwa kwa tuhuma gani na amepekuliwa nyumbani kwake kwa lengo la kutafuta ushahidi gani.

Hata hivyo, mtandao huu ulipomtafuta Kamishna Sirro, amejibu kwa kifupi “Mimi bado sina taarifa za jambo hilo, ngoja nifuatilie.”

MwanaHALISI Online imemtafuta Askofu Gwajima kwa njia ya simu, hata hivyo hakupatikana.

Askofu Gwajima aemkuwa katika mvutano na Paulo Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam tangu Makonda alipomtuhumu kujihusisha na dawa za kulevya na hivyo kushikiliwa na jeshi la polisi  kwa siku mbili na kuhojiwa kabla ya kuachiwa.

Jumapili iliyopita Gwajima alijibu mapigo kwa kusema Makonda alimtaja yeye kutokana na hofu kuwa Askofu huyo anaweza kuwania ubunge katika Jimbo la Misungwi, Mwanza ambalo hata RC huyo anajipanga kugombea.

Alienda mbali na kusema jina halisi la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ni Daudi Albert Bashite na kwamba jina lake la sasa limetokana na kuchukua cheti cha kidato cha nne cha mtu anayejulikana kama Paulo Christian.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!