Saturday , 25 March 2023
Home Kitengo Michezo Ukata wamuondoa Pluijm Yanga
Michezo

Ukata wamuondoa Pluijm Yanga

Hans van Pluijm
Spread the love

KLABU ya Yanga imesitisha mkataba wa aliyekuwa Mkurugenzi wa Ufundi, Hans Van Der Pluijm kutokana na klabu hiyo kutokuwa na uwezo wa kuendelea kumlipa, anaandika Erasto Masalu.

Pluijm alikuwa Kocha Mkuu wa klabu hiyo kwa misimu miwili kabla ya kupandishwa na kuwa mkurugenzi wa ufundi wa klabu hiyo, lakini sasa amefunguliwa milango ya kuondoka.

“Nimepewa barua asubuhi hii na Yanga juu ya mkataba wangu kuwa umesitishwa. Walichokisema ni kuwa klabu kwa sasa ina Ukata na hawana uwezo wa kuendelea kunilipa,” amesema Pluijm.

“Kwa sasa nipo huru kujiunga na klabu yeyote itakayoonyesha nia na mimi basi nitafanya nao kazi.” Alisisitiza Pluijm.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

Michezo

Kimwanga CUP yazidi kutimua vumbi

Spread the loveMASHINDANO ya mpira wa miguu ya Kimwanga CUP ya kuwania...

error: Content is protected !!