Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu agoma kula, ashinikiza kupelekwa mahakamani
Habari za Siasa

Lissu agoma kula, ashinikiza kupelekwa mahakamani

Wakili Peter KIbatala (kushoto) akijadili jambo na mteja wake, Tundu Lissu, Mbunge wa Singida Mashariki
Spread the love

TUNDU Lissu, Mbunge wa Singida Mashariki na Mwanasheria Mkuu wa Chadema, amegoma kula chakula kutwa nzima ya leo, akishinikiza kupeleka mahakamani, anaandika Faki Sosi.

Kwa mujibu wa wakili wa Lissu, Peter Kibatala, mteja wake amegoma kula toka asubuhi, mchana na jioni kwa madai hata fanya hivyo mpaka atakapopelekwa mahakamani.

“Mke wa Lissu alileta chakula asubuhi, lakini Lissu aligoma kula na kumwambia mkewe asihangaike kwani hatakuka mpaka atakapofikishwa mahakamani,” amesema Kibatala.

Kibatala amesema kwa sasa wanapigania mteja wake apelekwe mahakamani kwani muda wa kisheria kushikiriwa kituoni umemalizika.

Lissu alikamatwa jijini Dodoma nje ya viwanja vya Bunge, Februari 6, 2017 na kuletwa Dar es Salaam katika kituo cha Polisi cha Kati kwa mahojiano, huku kosa lake likidaiwa ni kauli za uchochezi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

error: Content is protected !!