Sunday , 28 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Polisi Dar kuwavaa wauza silaha
Habari Mchanganyiko

Polisi Dar kuwavaa wauza silaha

Mapanga yakiwa yanauzwa barabarani
Spread the love

JESHI la Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewataka wafanyabiashara kuacha kuuza silaha kama mapanga, majambia, visu, manati na upinde bila utaratibu wa kisheria, anaandika Pendo Omary.

Simon Sirro, Kamishna wa Polisi leo amewaambia waandishi wa habari kuwa biashara hiyo kwa sasa imeshamiri katika barabara ya Nyerere/Tazara kwenye mataa ya kuongoza magari, Chang’ombe na gerezani hali inayohatari usalama wa watu hususan watumiaji wa barabara hizo.

“Baadhi ya wauzaji wa bidhaa hizo, hutumia fursa hiyo kuwatishia watu wakiwa kwenye magari binafsi na yale ya umma na kuwaibia mali mbalimbali kama simu za mkono, saa, mikoba, pochi na kompyuta mpakato,” amesema Sirro.

Sirro amesema silaha hizo zinatakiwa kuuzwa kwenye maduka yenye leseni na kwamba atakayepatikana akifanya biashara hiyo atachukuliwa hatua kali za kisheria.

“Tarehe 12 Januari mwaka huu, kwenye mataa ya Tazara alikamatwa mtuhumiwa Ngoli Salakani (39), akifanya biashara hiyo. Hatua za kisheria zinachukuliwa dhidi yake,” amesema Sirro.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NBC yapata tuzo ya mwezeshaji bora wa mikopo serikali Afrika

Spread the loveBenki ya NBC imepata tuzo ya Mwezeshaji Bora wa Pamoja...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Biteko aipongeza GGML kudhibiti vifo, majeruhi mahali pa kazi

Spread the loveNAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari Mchanganyiko

Wami Ruvu hawana deni la Rais Samia katika kutunza vyanzo vya maji

Spread the love  BODI ya Maji Bonde la Wami Ruvu, imeendelea kuchua...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

error: Content is protected !!