Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa 1.5 Trilioni zipo wapi?
Habari za Siasa

1.5 Trilioni zipo wapi?

Spread the love

SI Bunge wala wananchi wanaojua kiasi cha Sh. 1.5 Trilioni ambazo hazikuonekana kwenye Ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali ya 2016/17 zilipo. Anaripoti Yusuph Katimba…(endelea).  

Serikali kwenye Bunge hili la 14 itakuwa na kibarua cha kueleza umma matumizi ya fedha hizo ambapo ndani ya taarifa ya CAG 2016/17 haikueleza matumizi yake.

Mwanasiasa Zitto Kabwe, ambaye ni Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), ndiye aliyeibua suala hilo na kulivalia njuga wakati wa vikao vya Bunge la Bajeti.

Zitto, aliyedai kutumia ripoti ile ile ya CAG inayoishia Juni 30, mwaka juzi, alihoji ziliko Sh trilioni 1.5.

Hata hivyo, hoja ya Zitto ilijibiwa Aprili 20, mwaka jana na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji, aliyefafanua kuwa, katika fedha hizo kiasi cha Sh bilioni 697 kilitumika kwa matumizi ya dhamana na hati fungani zilizoiva na Sh bilioni 687 kilikuwa kwa ajili ya mapato tarajiwa.

Pia alisema kiasi cha Sh bilioni 203 kilikusanywa kama kodi kwa niaba ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ).

Baada ya sakata hilo kuibuliwa tena bungeni Juni 5 mwaka jana na wabunge wa Chadema, Halima Mdee (Kawe) na John Mnyika (Kibamba) kulisababisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu), Jenista Mhagama, kuwataka wabunge kutojadili kuhusu fedha hizo ndani ya Bunge hadi hapo PAC inayoifanyia kazi itakapowasilisha ripoti yake.

Kutokana na sakata hilo, Rais Dk. John Magufuli alimhoji CAG, Profesa Musa Assad na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dotto James, kuhusu ukweli wa madai ya upotevu wa fedha wakati alipowaapisha majaji wapya walioteuliwa Ikulu, Dar es Salaam na wote kwa pamoja walikanusha.

Mijadala ndani na nje ya Bunge n ahata ndani ya Ikulu haikuweza kutoa melezo yanaokinahisha zilipo fedha hizo. Miongoni mwa kazi kwenye Bunge hili la 14 ni kujadili ripoti hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!