Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto atinga ofisi za CUF, ajifungia na Maalim Seif
Habari za Siasa

Zitto atinga ofisi za CUF, ajifungia na Maalim Seif

Spread the love

ZITTO Kabwe, Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo leo tarehe 18 Machi 2019 amefika katika Ofisi ya Wabunge wa Chama cha Wananchi (CUF) Magomeni jijini Dar es Salaam kuzungumza na Maalim Seif Shariff Hamad. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Zitto ambaye ni Kiongozi Mkuu wa ACT-Wazalendo alifika ofisini hapo muda mfupi baada ya Maalim Seif, aliyekuwa Katibu Mkuu wa CUF kutangaza kujiunga na ACT-Wazalendo.

Kufika kwa Zitto ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Mjini kulipokewa kwa shangwe na baadhia ya viongozi waliokuwa wa CUF na wanaomuunga mkono Maalim Seif.

“ACT-Wazalendoooo, ACT-Wazalendoo” ndio maneno yaliyokuwa yakitamkwa na viongozi hao wakati wakimpokea Zitto ambaye baada ya kufika, alipelekwa moja kwa moja chumba alichokuwemo Maalim Seif.

Humo ndani Zitto na Maalim Seif walitete kwa dakika kadhaa na kisha Zitto kutoka na kupanda gari lake kisha kutokomea. Haijaelezwa Zitto na Maalim Seif walizungumza nini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!