Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto atinga ofisi za CUF, ajifungia na Maalim Seif
Habari za Siasa

Zitto atinga ofisi za CUF, ajifungia na Maalim Seif

Spread the love

ZITTO Kabwe, Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo leo tarehe 18 Machi 2019 amefika katika Ofisi ya Wabunge wa Chama cha Wananchi (CUF) Magomeni jijini Dar es Salaam kuzungumza na Maalim Seif Shariff Hamad. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Zitto ambaye ni Kiongozi Mkuu wa ACT-Wazalendo alifika ofisini hapo muda mfupi baada ya Maalim Seif, aliyekuwa Katibu Mkuu wa CUF kutangaza kujiunga na ACT-Wazalendo.

Kufika kwa Zitto ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Mjini kulipokewa kwa shangwe na baadhia ya viongozi waliokuwa wa CUF na wanaomuunga mkono Maalim Seif.

“ACT-Wazalendoooo, ACT-Wazalendoo” ndio maneno yaliyokuwa yakitamkwa na viongozi hao wakati wakimpokea Zitto ambaye baada ya kufika, alipelekwa moja kwa moja chumba alichokuwemo Maalim Seif.

Humo ndani Zitto na Maalim Seif walitete kwa dakika kadhaa na kisha Zitto kutoka na kupanda gari lake kisha kutokomea. Haijaelezwa Zitto na Maalim Seif walizungumza nini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!