Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Yametimia; Prof. Assad atua bungeni na ushahidi wake
Habari za Siasa

Yametimia; Prof. Assad atua bungeni na ushahidi wake

Prof. Mussa Assad, Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali. Picha ndogo Job Ndugai, Spika wa Bunge
Spread the love

MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Prof. Mussa Assad, tayari yupo Dodoma “kukabiliana” na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Kinga, Maadili na Madaraka ya Bunge, kufuatia Spika wa Bunge la Jamhuri, Job Ndugai, kutoa amri ya kufika mbele ya kamati hiyo. Anaripoti Danson Kaijage, kutoka Dodoma … (endelea).

Prof. Assad anatuhumiwa na Spika Ndugai, kulidhalilisha Bunge, kufutia kauli yake kuwa mhimili huo wa kutunga sheria, ni “dhaifu.” 

Hata hivyo, Prof. Asaad amekana madai hayo. Amesema, “neno dhaifu, ni neno la kawaida, tena la kiungwana kabisa, kwa wataalam wa mahesabu na limekuwa likitumika mara kadhaa katika kuripoti kazi za taasisi yangu.”

Aidha, Prof. Assad alisema kuwa alichokieleza alipokuwa nchini Marekani wakati akihojiwa na Idhaa ya Kiswadili ya Umoja wa Kimataifa (UN), ni maoni yake binafsi na akataka maoni hayo yaheshimiwe kwa mujibu wa Katiba.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa maofisa wa Bunge mjini hapa, Prof. Assad anatarajiwa kuingia ndani ya Kamati hiyo, majira ya saa nne na nusu asubuhi hii ya leo, tarehe 21 Januari.

Prof. Assad aliyeingia madarakani mwaka 2014 wakati wa utawala wa Rais Jakaya Mrisho Kikwete, alieleza katika mahojiano yake hayo na radio ya Umoja wa Mataifa (UN), kuwa kushindwa kufanyiwa kazi kwa ripoti ya ofisi yake kunatokana na “udhaifu wa bunge,” jambo ambalo linadaiwa kumkasirisha Spika Ndugai.

Alisema, “…kama tunatoa ripoti na kuna ubadhirifu na hatua hazichukuliwi, huo kwangu ni udhaifu. Bunge linatakiwa lisimamie na kuhakikisha kwamba pale kwenye matatizo hatua zinachukuliwa.”

Alikuwa akihojiwa na mwandishi wa Idhaa ya Kiswahili ya radio hiyo, Anord Kayanda, aliyetaka kujua sababu za ripoti zake kutofanyiwa kazi na Bunge.

Kamati ya Haki, Kinga, Maadili na Madaraka ya Bunge, inaongozwa na Mbunge wa Tabora Mjini (CCM), Emmanuel Adamson Mwakasaka.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka ofisi ya katibu wa Bunge, mara baada ya Prof. Assad kuripoti bungeni, atakwenda moja kwa moja kwenye ukumbi wa mahojiano uliyopo jingo la utawala na kisha kusomewa mashitaka yanayomkabili na mwanasheria wa Bunge.

Baada ya kusomewa mashitaka hayo, kanuni zinamtaka kujibu au kutojibu lolote na akiamua kujibu, ndipo wajumbe wa kamati hupata nafasi ya kumuuliza maswali.

Taarifa zinasema, baada ya Kamati kumaliza kazi yake, wanawasilisha mapendekezo ya adhabu; na au ushauri kwa Spika ambaye anaweza kuamua kuletwa bungeni ili kujadiliwa au kulimaliza jambo hilo kupitia ofisi yake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!