Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Vodacom wamponza Mkurugenzi TCRA
Habari za Siasa

Vodacom wamponza Mkurugenzi TCRA

Mhandisi Izack Kamwelwe, Waziri wa Uchukuzi, Usafirishaji na Mawasiliano. Picha ndogo, Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Mhandisi James Kulaba
Spread the love

MHANDISI Izack Kamwelwe, Waziri wa Uchukuzi, Usafirishaji na Mawasiliano amempa siku 30 Mkurugenzi wa Mawasiliano Tanzania  (TCRA) kuzungumza na Kampuni ya Mtandao wa simu ya  Vodacom Tanzania kutatua kero ya wizi wa fedha unaofanya kupitia mtandao huo. Anaripoti Khalifa Abdallah … (endelea).

Kamwelwe amesema hayo leo akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za TCRA wakati kampuni hiyo ikipatiwa leseni ya Masafa marefu ya 700MHz itakayowezesha kutanua wigo wa mawasiliano kwa kampuni hiyo.

“Nendeni mkakae mfikirie kabla sijatoa maelekezo ili mtu akiniibia kwenye simu yangu kwenye yangu ya Vodacom kampuni iwajibike kurudisha, mna wafanyakazi ambao wapo nje ya mfumo, lakini lazima mliwaajiri na mkawafukuza hao ndiyo wanaotuibia,” amesema Kamwelwe.

Katika hatua nyingine Kamwelwe amesema kuwa daraja la kisasa la Salander linalotarajiwa kujengwa na Tanzania katika barabara inayotokea Coco Beach hadi kutokea Agha Khan ni daraja la kwanza kutokea Tanzania.

Daraja hilo lililogharimu Dola za Marekani 126 milioni linatarajiwa kuwa ni urefu wa Km 1 na Mita 30.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!