MHANDISI Izack Kamwelwe, Waziri wa Uchukuzi, Usafirishaji na Mawasiliano amempa siku 30 Mkurugenzi wa Mawasiliano Tanzania (TCRA) kuzungumza na Kampuni ya Mtandao wa simu ya Vodacom Tanzania kutatua kero ya wizi wa fedha unaofanya kupitia mtandao huo. Anaripoti Khalifa Abdallah … (endelea).
Kamwelwe amesema hayo leo akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za TCRA wakati kampuni hiyo ikipatiwa leseni ya Masafa marefu ya 700MHz itakayowezesha kutanua wigo wa mawasiliano kwa kampuni hiyo.
“Nendeni mkakae mfikirie kabla sijatoa maelekezo ili mtu akiniibia kwenye simu yangu kwenye yangu ya Vodacom kampuni iwajibike kurudisha, mna wafanyakazi ambao wapo nje ya mfumo, lakini lazima mliwaajiri na mkawafukuza hao ndiyo wanaotuibia,” amesema Kamwelwe.
Katika hatua nyingine Kamwelwe amesema kuwa daraja la kisasa la Salander linalotarajiwa kujengwa na Tanzania katika barabara inayotokea Coco Beach hadi kutokea Agha Khan ni daraja la kwanza kutokea Tanzania.
Daraja hilo lililogharimu Dola za Marekani 126 milioni linatarajiwa kuwa ni urefu wa Km 1 na Mita 30.
Leave a comment