Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Vita ya ruzuku CUF yatinga Mahakama ya Rufaa
Habari za SiasaTangulizi

Vita ya ruzuku CUF yatinga Mahakama ya Rufaa

Spread the love

BODI ya Wadhamini ya CUF imefungua shauri Na. 343/01/2018 katika Mahakama ya Rufaa, kupinga amri ya zuio la kutolewa ruzuku ya chama hicho iliyotolewa na Mahakama Kuu. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Bodi hiyo iliyo chini ya Mwenyekiti anayetambuliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Profesa Ibrahim Lipumba, iliwakilishwa na Peter Malebo, Thomas Malima na wengine 7, ambapo leo tarehe Mosi Novemba 2018, shauri hilo lilisikilizwa mbele ya jopo la majaji watatu wakiongozwa na Jaji Mussa Kipenka, Jaji Richard Mziray na Jaji Gerald Ndika.

Jopo la Majaji watatu wa Mahakama ya Rufaa itatoa hukumu juu ya hoja za awali za mapingamizi baada ya kutoa taarifa (NOTICE) kama ulivyo utaratibu wake. Na kwamba, kwa mujibu wa kanuni za Mahakama ya Rufaa hukumu inatarajiwa kutolewa ndani ya siku 14 kuanzia tarehe shauri liliposikilizwa.

Katika maombi yake ya msingi, bodi hiyo inaiomba mahakama ya rufaa kutengua uamuzi katika shauri Na. 80/2017 lililofunguliwa kwenye Mahakama Kuu Oktoba 2017, na Bodi ya Wadhamini inayomuunga mkono Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad.

Mahakama Kuu mbele ya Jaji Wilfred Dyansobera ilitoa amri ya kumzuia Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi kutoa fedha za ruzuku ya CUF kwa Pro. Lipumba na wenzake, hadi pale maamuzi ya shauri Na. 21/2017 dhidi yake na Mwanasheria Mkuu wa Serikari (CAG) kuhusu tuhuma za kutoa fedha za ruzuku Sh. 369 milioni, yatakapotolewa.

Kesi hiyo ilifunguliwa na Bodi ya Wadhamini ya CUF inayomuunga mkono Maalim Seif, ikidai kuwa fedha hizo hazijulikani matumizi yake, pamoja na kutokuwa kwenye mikono salama kutokana kwamba Prof. Lipumba ambaye bodi yake ilikabidhiwa fedha hizo, alivuliwa uanachama.

Mvutano wa bodi hizo mbili ulikuja baada ya uwepo wa mgogoro wa kiungozi uliokikumba chama hicho, ambapo upande wa Maalim Seif unadai kuwa Prof. Lipumba si mwenyekiti halali kufuatia kuvuliwa uanachama wa CUF, wakati Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa na Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) ikimtambua kuwa kiongozi halali pamoja na bodi yake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!